Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba niseme mambo machache na ninaomba Mheshimiwa Waziri unisikilize kwa makini kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza mwaka jana kuna vijana wamepotea katika Jimbo langu la Serengeti, walikamatwa porini vijana zaidi ya 20, mpaka leo ninavyoongea ndugu zao wamewatafuta hawajulikani waliko. Inasemekana wameuawa na askari wa wanyama pori, unapokuja hapa niambie wako wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, Mheshimiwa Waziri unakumbuka walikuja hapa Wajumbe wa WMA mwaka huu, walikuja Madiwani, walikuja Wenyeviti wa Serikali za Vijiji, walikuja na baadhi ya watendaji kwa ajili ya tatizo la single entry! Sasa tulikutana na wewe ukasema Kamati imekataa. Inawezekana Kamati imeamua, imechukua maamuzi haya kwa sababu haijafika Serengeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye mapori ya akiba ya Ikorongo na Grumet Game Reserve pamoja na WMA ya Ikona, jiografia ya kwake ni tofauti kabisa na WMA ambazo ziko maeneo mengine.
Mimi ninakuomba Mheshimiwa Waziri tusaidiane wote na Kamati iende ikakutane na Wajumbe wa Ikona WMA, otherwise you want to kill WMA! Na WMA ikifa pale maana yake mapori ya akiba yale yote yataangamia. Maana kama yataangamia maana yake hakuna ajira. Vijana wataanza kuwinda, no conservation will proceed there. Kwa hiyo, ninakuomba Mheshimiwa Waziri fanya juu chini, Kamati yako itembelee Serengeti ili ikajiridhishe nini kilio cha watu wa pale Serengeti, lakini kama mkikaa hapa mezani mkaamua, kule mtaua yale mapori na hakuna kitakachoendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu, Serengeti National Park imeanzishwa kwa mujibu wa sheria na imekuwa Gazzeted kwenye Gazeti la Serikali tangu mwaka 1968 kwenye GN Na. 235; ukisoma ile GN iko clear, inataja mipaka ya Hifadhi ya Serengeti National Park. Kilichotokea Wizara yako imeendelea ku-extend mipaka kila kunapoitwa leo. Tangu GN itangazwe wame-extend mipaka zaidi ya mitano, wamechukua maeneo ya wananchi. Sasa sielewi nini maana ya GN? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama GN imetangaza mipaka, leo Wizara yako ina-violate, inachukua maeneo ya wananchi na bahati nzuri beacon zilipo zote tunazifahamu sisi watu wa Serengeti na Mheshimiwa Waziri ukitaka tutakuonesha. Naomba kitu kimoja, unapokuja naomba uniambie uko tayari wewe na Waziri wa Ardhi Mheshimiwa Lukuvi, kwenda kuhakiki mipaka ambayo ilitangazwa kwenye GN mwaka 1968? Ninataka hayo majibu wakati unapokuja kujumuisha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni tembo na simba. Nimepiga kelele sana kwenye maswali na imefikia sehemu ninaitwa tembo. Iko hivi, hakuna watu wanaopata shida kama wananchi wa Serengeti dhidi ya tembo na simba. Tembo siku hizi anatembea tu kama binadamu wa kawaida, mnagongana naye kama binadamu wa kawaida, hakuna mtu anayechukua hatua dhidi ya tembo na simba. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, siku moja simba wamevamia kijiji cha Park Nyigoti, sasa wananchi siku hizi walishaelewa ili askari waje hawasemi simba amekamata mnyama, wanapiga simu wanasema tumeuwa simba hapa, dakika tano haziishi wameshafika. Kwa hiyo maana yake ni nini! Tembo, simba ni wa thamani kuliko binadamu. (Kicheko)
Sasa Mheshimiwa Waziri nataka pia unapokuja hapa utuambie katika Sheria ya Wanyamapori mko tayari ku-review, kuileta hapa Bungeni tuipitie upya vile viwango vya kifuta machozi na kifuta jasho? Maana tunajua hamtoi fidia. Mnatoa kifuta machozi na kifuta jasho ambavyo kimsingi haviendani na wakati tulionao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tembo wamekula mashamba ekari tano unampa mtu shilingi 100,000 for what? Shilingi 100,000 kwa eka tano shilingi 100,000 inatosha hata kwa mbegu? Mtu akiuawa mnampa shilingi 1,000,000 hata hiyo shilingi 1,000,000 ataomba miaka 10 ndiyo mnampa. Wewe ni shahidi unafahamu, hamjawahi kulipa. Pale Serengeti watu wameuawa wengi sana na tembo, sijawahi kuona mtu amelipwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi nimeona wameleta wanalipa laki moja moja kwa baadhi ya watu, wengine wote walioathirika hakuna.
Sasa naomba unapokuja ku-wind up uniambie ni lini utaleta ile sheria tuipitie, kifuta machozi, kifuta jasho ili kiendane na wakati tulionao? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu barabara. Mimi sijawahi kuona, ninasikia sijatembea sana, lakini nasikia kuna Mbuga inaitwa Kruger iko Afrika ya Kusini, ukitembea kwenye ile mbuga na wanasema ndiyo mbuga inayoingiza watalii wengi na ndiyo mbuga inaingiza mapato mengi, lakini ukienda kwenye mbuga ile kuna lami. Wale ambao mmefika mtakuwa mashahidi, lakini kwenye Mbuga yetu ya Serengeti, hiyo hakuna! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda Serengeti ukianzia Tarime, watalii wengi wanatokea Tarime, Sirari. Barabara ile watalii wanalalamika kila leo ingawa ninyi mnapuuza lakini watalii wanalalamika. Wanahitaji kutembelea Serengeti, lakini kutokana na barabara mbovu zilizopo wanaogopa.
Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri, gharama ambayo mnaitumia kila siku ku-maintain barabara za hifadhini ni afadhali mngeangalia zile barabara za msingi, zile ambazo zinatumiwa na magari mkaziwekea lami, hizo nyingine za kawaida kwa sababu hazina magari mazito, mnaweza kuzi-maintain kwa kutumia kifusi na kawaida. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ukija kwenye Mbuga ya Wanyama ya Serengeti National Park kuna hoteli lukuki, zaidi ya hoteli 100 ziko mle. Kuna camp nyingi lakini hayalipi service levy wamekimbilia mahakamani yet Serikali mko hapa, hamzisaidii Halmashauri zetu kupata mapato! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, unapochukulia Halmashauri kama Wilaya ya Serengeti kwa muda mrefu hatunufaiki na utalii. Inafikia sehemu watu wanakata tamaa. Sasa hakuna wananchi wenye nidhamu kama wananchi wa Serengeti kwenye conservation. Huwa wanakuja pundamilia (zebra), tunawarudisha, tunawapigia simu wanakuja wanawachukua. Wananchi wana nidhamu kweli, lakini itafikia sehemu tutachoka. Hebu tusaidie Mheshimiwa Maghembe tupate service levy! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, mkatunyang‟anya na bed fee, gate fee unajua ya kwamba Serengeti mizigo tunayoipata, vitu vya madukani tunavyovipata tunatoa Arusha, lakini mnawa-charge wafanyabiashara wa Serengeti kwenye mageti ya Ikoma Gate, wapi huko kwenda Ngorongoro wanachajiwa (charge) gharama kubwa! Vitu Serengeti ni bei ya juu kweli kweli. Mfuko wa saruji ninavyoongea sasa hivi ni shilingi 23,000 nadhani ndio inaongoza…
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Chacha.