Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa mara ya kwanza nimeitwa jina ninalolipenda la Albeto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo machache ya kuzungumzia na kwanza nitaanza na mjusi, Wajumbe wengi humu wamepiga kelele juu ya mjusi kwamba, kwa nini harejeshwi Tanzania! Mimi ni katika wale ambao wanaunga mkono arejeshwe, lakini najiuliza kama tuko tayari kumpokea na tunaweza kumtunza; lakini kumrudisha tunaweza. (Makofi)
Mheshimmiwa Mwenyekiti, tayari kuna international precedents nyingi zimetokea za mali ambazo zimechukuliwa katika nchi na zikarudishwa. Mfano wa karibuni kabisa ni wa Ethiopia, kuna mnara unaitwa Obelisk, umri wake ni karibu miaka 1700 na una urefu wa mita kama 24, ulikuwepo Italia kwa miaka 68. Baadaye Ethiopia wameweza kuurudisha na upo nchini kwao na ni sehemu ya utalii wao. Sasa inategemea kama Serikali tunaweza ku-negotiate tukaweza kumrudisha. Hata hivyo, kabla ya hapo ningependa sana tutengeze mazingira ili mjusi huyo asije akaozea kwetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni suala la utalii nitalizungumza kwa undani kidogo kwa sababu ni area ambayo naielewa vizuri zaidi. Kwanza, ningetaka kusema kwamba, tuna haja ya kushambulia emerging markets, emerging markets, markets mpya hizi za China, Urusi, India, Arabia, ni sehemu ambazo zinatengeneza pesa sana na hata ukilinganisha namna ambavyo wanatengeneza mamilionea per day wao wako mbele. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni namna gani utatumia kuwavutia kuja kwetu? Nitatoa mfano mdogo wa namna ambavyo kama tutaweza kufaidika na emerging markets, mfano nitakaotoa ni wa Mauritius. China katika mwaka 2011 walipeleka watalii 15,000 Mauritius. Mwaka uliofuata walipeleka watalii 22,000, mwaka mwingine walipeleka watalii 14,000 na mwaka 2014 wakapeleka watalii 63,000 na ushee. Mwaka 2011 India walipeleka watalii 53,000, ikawa 55,000, ikawa 57,000, ikawa 61,000 na naamini tukisema hivi sasa rate yao itakuwa imepanda. Kwa hivyo, namshauri Mheshimiwa Waziri kwenye Wizara yake ajaribu kwenye emerging markets, hilo la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ni suala la re-branding Tanzania. Tanzania tumepitia process mpya kubwa na ndiyo maana hata tukaona kuna haja ya kufanya katiba mpya kwa sababu kama nchi tumepitia mambo mengi lazima tujitambulishe upya kama Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, branding ambayo tunayo hivi sasa ndiyo ambayo kwa miaka yote imetupa watalii milioni, labda 1,200,000. Hii branding nataka ifanywe upya tujitambulishe tuna vitu gani vya kuuza, vinapatikana wapi, vinapatikana vipi, rates zetu ziko vipi. Kwa mfano, tumetumia brand ya Tanzania, land of Kilimanjaro and Zanzibar kwa miaka yote hiyo, tumepata watalii 1,100,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunashindwa kupata watalii zaidi kwa sababu sisi hatutaki kujilinganisha na wengine, sisi tuna vivutio vingi, Mauritius wana vivutio vichache kuliko sisi lakini wao wanatupita, wao tayari 2014 walikuwa wana watalii 1,200,000. Ni kisiwa cha watu 1,500,000 lakini wamepata watalii 1,200,000. Kwa hivyo kuna haja ya ku-re-brand. Lakini hiyo re- branding tusiifanye sisi tuwape watu, mashirika makubwa wanaoweza kufanya re-branding ili tuweze kupata faida. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hiyo hiyo na sasa nataka nizungumzie habari ya re-discovering our pontentials. Watu wengi wamezungumza hapa, kuna watu wamezungumza kwamba, inaonekana kama kuna upendeleo au ndiyo culture tuliyoachiwa, kwamba utalii ni kaskazini. Lakini kuna southern circuit ambayo inaweza ikatusaidia sana. Pia kuna sehemu nyingine za pembezoni, kwa mfano Mara, Arusha wameungana na Kenya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tumejipanga vipi sisi utalii wetu kuungana na Uganda, tumejipanga vipi utalii wetu kuungana na Mozambique, kuungana na sehemu nyingine ambazo tunapakana nazo. Nitatoa mfano wa Kagera, kagera tuko na Uganda. Lazima tuwe na package ambayo inamfanya mtu akienda Uganda baadaye akija Kagera ashawishike. Juzi nilifunuliwa macho na Profesa Tibaijuka hapa aliposema kuna ziwa linaitwa Ziwa Burigi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiambiwa chochote dakika ile ile nakwenda kwenye internet. Pale pale nikaenda kwenye internet nikaona how beautiful that place is. Ni mahali ambapo mtu yeyote angeweza kwenda. Tuna game reserve ya Burigi lakini tuna ziwa, lakini hakuna hata kibanda cha mtalii kufika. Pale kwa nilivyosoma na nimetamani, nimemwambia mama Mwigaje hapa nataka niende nikaone, ile picha niliyoipata Ziwa Burigi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo tunaweza tukamshawishi mtalii kutoka Uganda akaja pale, hali kadhalika southern circuit. Kuna fursa nyingi beach sun mpya za Mtwara na Lindi, mnazitumiaje kama sehemu ya southern circuit. Kwa hiyo, tubadilike katika hilo.
Mheshimwa Mwenyekiti, halafu nataka kuzungumzia juu ya advertising. Nchi kama Malaysia, Indonesia, zimepiga hatua kubwa sana katika utalii, lakini bado wanatangaza costing millions to them. Tangazo lao linapendeza, unalipenda, unalisikiliza. Kwa hivyo lazima tuchukue international firms siyo tunapeleka tangazo kwenye Sunderland ambalo linawekwa tu hivi. Tangazo lazima liwe strategic, idadi ya watu wangapi, tunafaidika vipi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija katika nukta hii hii nataka nizungumzie Walking billboard. Tuna Mbwana Samata anacheza mpira Belgium, kwa nini kama Taifa au kama Wizara tusiingie naye mkataba akifunga goli akiinua jezi tu visit Tanzania, ambayo inaonekana dunia nzima na sio Belgium tu, lakini hatutumii potential tulizonazo. Kwa hivyo, ningependa hili tulitazame. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna sports tourism. Nilizungumza na Mheshimiwa Nape juu ya namna ya sisi kujipanga kama Taifa. Nchi hii hakuna international tournament ya golf, hakuna international tournament ya Tennis, hakuna international tournament ya cycling. Nchi kubwa lakini haijajipanga vyovyote vile kimichezo. Kwa hivyo, ningependa kwamba, eneo hilo pia tulitengeneze ili tuweze kuzitumia vizuri tufaidike. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nataka nizungumzie role mpya ya Mabalozi. Mabalozi wote lazima waelekezwe kwamba, hivi sasa tutengeneze tourism diplomacy kuwe na package, watayarishwe, wawekewe na malengo namna ambavyo wanaweza kukuza utalii wetu; lakini isaidie kwamba, watengenezewe package ili tuweze kufaidika ndani ya nchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa, nataka nizungumzie suala la kutengeneza mnaso wa community kubwa ya wageni wanaoishi maeneo ya East Africa. Mzungu au expert yeyote ambaye yuko East Africa unamtoza visa sawasawa na ambaye amekuja leo kutoka Marekani. Tuwe na package maalum ya expertise kutoka Rwanda, Kenya, Uganda, tuwe na package maalum washawishike kuja kwetu. Mtu mmoja alisema lazima tuweke rates za kuvutia ili watu waje, baadaye tuweze kubadilisha lakini lazima tu-change katika strategy hizi na kwamba, tunatoza kodi nyingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ni very expensive destination, tusijisifu kwa watu wanaokuja, tungeweza kupata watu zaidi kama tutajitengeneza vizuri zaidi. Sisi ni losers, hatuna haja ya kushindana na Kenya, hatuna haja ya kushindana na Uganda, tuweke rates ambazo zinatufaidisha sisi na ndiyo maana tutawashinda. Ndiyo maana kukitokea matatizo Kenya sisi tunafaidika. Kwa hiyo, tusingojee mpaka Kenya wapigane sisi tufaidike. Pia tunaweza tukaweka rates ndogo ili tuvutie watalii zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumalizia ningependa kuzungumzia habari ya standards. Tunakwenda nchi za wenzetu, tuna hotel higher lakini unaona kwamba, bado tuko nyuma, service mbovu. Ningependa tuhakikishe kwamba, tunakuza sekta kwa kuwa hata na masomo ya degree na tuweze …
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Alberto.