Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia bajeti hii ya Wizara ya Maliasili na Utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, napenda tu nimshauri Mheshimiwa Waziri ili anapokuja wakati mwingine kwa sababu hii ni bajeti yake ya kwanza ajaribu sana kuangalia yale masuala ambayo ni controversial ili yaweze kuingia kwenye taarifa tusiwe na kuhoji wala kushauri kwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naomba nijikite katika masuala machache sana kutokana na muda wenyewe kuwa mfupi. La kwanza ni katika sekta hii ya utalii ambapo Serikali inapata pato la Taifa asilimia 17.5, ile GDP. Hii ingeweza kuongezeka zaidi lakini inategemea na matatizo ambayo wanayo wale tour operators wetu ambao wako nchi za nje kwa maana ya kwamba ile package wanayochaji pesa za nje zinabaki kule Serikali inapata kiduchu, inaambulia patupu. Naomba Mheshimiwa Waziri anapokuja hapa atuletee mikakati ambayo itakuwa ina tija ili Serikali iweze kupata pesa nyingi zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, hapa Waheshimiwa wengi wanazungumzia suala la concession fee, ni kweli hili jambo Serikali imekuwa ikipoteza fedha nyingi sana na kama tunavyoelewa TANAPA ni shirika kubwa sana na linafanya kazi nzuri sana. Pamoja na hayo, ninachoelewa ni kwamba TANAPA wameshatoa mapendekezo yao kwa ajili ya kuongezea pato Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, lazima tujiulize Waheshimiwa wengi wamesema concession fee imechukuwa muda mrefu hivyo, TANAPA mpaka leo hii, zaidi ya miaka miwili na nusu haina Bodi, masuala mengine hata hili suala la concession fee haliwezi kufanyika bila Bodi ku-approve. Kwa hiyo, pamoja na kwamba suala la Bodi pia Mwenyekiti lazima ateuliwe na Rais, ni jukumu la Mheshimiwa Waziri kama mwenye dhamana kuhakikisha kwamba ana-push TANAPA iweze kuwa na Bodi ili masuala mengine kama haya ya concession fee yaweze kwenda mbele. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo hapo katika Shirika hili la TANAPA, Wabunge wengi hapa ndani wamelipongeza. Ni kweli linafanya kazi vizuri, wote ni mashahidi tunajua kabisa kwamba katika programu yao ya CSR, mikoa 16, wilaya zaidi ya 55 zinazopakana na hifadhi wamechangia madawati shilingi bilioni moja, hii ni kazi nzuri. Kama vile haitoshi bado TANAPA ni mojawapo ya mashirika machache ambayo yanachangia gawio kubwa sana kwa Serikali. Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja katika suala zima la misitu. Waheshimiwa wengi hapa wamechangia, utoaji vibali vya uvunaji ni jipu. Ni jipu kwa sababu hili limekuwa ni tatizo kubwa sana, huko hakujakaa vizuri kabisa, wananchi wanalanguliwa vibali vya uvunaji, vinatolewa kwa kujuana, wanauziana wale wale, vibali hewa. Mheshimiwa Waziri asipokaa vizuri hapa tunamtolea shilingi maana sisi wengine tunatoka katika Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini. Kwa hiyo, tunataka mkakati wa kina katika suala zima la utoaji wa vibali vya uvunaji na mbinu mbadala tunataka iwepo na yenyewe atuletee majibu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposema pesa nyingi zinapotea katika sekta hii ya utalii tunamaanisha. Pale Ngorongoro, pamoja na mengineyo, suala zima lile la smart card kwenye gate fees ni tatizo. Naomba Mheshimiwa Waziri anapokuja hapa atueleze pia suala la smart card kwenye gate fees likoje? Maana vilevile pale kuna utata, pesa nyingi sana inapotea, hili jambo ni very serious na lishughulikiwe mara moja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nije katika migogoro hii ya wakulima, wafugaji pamoja na hifadhi. Kwenye Bunge lililopita nilikuwa katika ile Kamati ya Operesheni Tokomeza Ujangili. Kwa hiyo, ninaposema hivi nina uhakika tulijionea nini katika suala zima la migogoro ya hifadhi, wakulima na wafugaji. Nawashukuru sana Waheshimiwa wengi ambao wamechangia hapa uhifadhi una maana yake, uhifadhi una umuhimu wake katika katika Taifa letu, wakulima wana umuhimu wake na wafugaji wana umuhimu wake, nini kifanyike hapa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi wote hapa tumetokana na uhifadhi, tumetokana na wakulima, tumetokana na wafugaji, lakini kila mtu akisimama akaanza kufagilia yale mambo ya kwake hatutafika hata huo uhifadhi pia utakufa. Kwa hiyo, nini kifanyike hapa, Waziri wa Maliasili awasiliane na Wizara ya TAMISEMI, Wizara ya Mifugo, Wizara ya Sheria, Wizara ya Ardhi pamoja na watalaam na watendaji wao, wakae chini, sheria ni msumeno, watuletee masuala ambayo yataleta tija, sheria itumike. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo, kuna wenzangu wengine hapa wameuliza kuhusu Operesheni Tokomeza Ujangili, Bunge lililopita sote ni mashahidi. Baada ya sisi kusoma ile taarifa yetu hapa, Mawaziri wanne wali-step down. Mheshimiwa Rais akaunda Tume ya Majaji mpaka leo hii hatujapata taarifa ili tuweze kujua haki ilitendekaje ama namna gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, muda wangu ni mchache, naomba niunge mkono hoja.