Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi na pole sana nimekusumbua sana kuku-remind kwa sababu ilikuwa nichangie asubuhi na nilifunga safari kutoka Jimboni kwa ajili hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri wa Wizara hii kwa sababu wiki iliyopita alifanya ziara na alifika kwenye Jimbo letu ambako kuna msitu mkubwa wa Sao Hill. Waheshimiwa Wabunge, huu ni msitu mkubwa katika Afrika Mashariki na Kati. Pia nipende kupongeza TANAPA kwa kutoa madawati, naamini na kule Mafinga yatafika. Lakini pia napenda kupongeza uongozi wa shamba la misitu ya Sao Hill kwa jinsi ambavyo tunashirikiana vizuri katika shughuli mbalimbali za kijamii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizi, sasa nijielekeze kuchangia. Kuna msemo kaa karibu na waridi na wewe uweze kunukia kama waridi. Sasa kule Mafinga bahati mbaya sana na Wilaya ya Mufindi kwa ujumla, tuko karibu na waridi ambao ni msitu wa Sao Hill lakini hatunukii kama waridi, kama alivyosema Mheshimiwa Kigola, tuko kwenye msitu lakini watoto wanakaa chini, sijui ni laana ya namna gani.
Kwanza ningependa kuzungumzia kuhusu vibali. Kuna mgao wa namna tofauti katika kutoa vibali, lakini utoaji wa vibali umegubikwa na ujanja ujanja usiokuwa na mfano. Niseme kabisa mwanzoni, kama sitapata maelezo mazuri wakati Mheshimiwa Waziri anahitimisha nitakusudia kutoa shilingi. Katika suala la vibali, kwanza kabisa kweli msitu huu ni wa Kitaifa lazima unufaishe Watanzania wote, lakini kama nilivyosema, kama unakaa karibu na waridi lazima unukie kama waridi. Msitu huu lazima kwanza uanze kuwanufaisha wale waliozungukwa na msitu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi babu yangu alikuwa Sub Chief wakati wa ukoloni. Sisi watu wa Mufindi, watu wa Mafinga tumetoa maeneo, tumepanda mitiā€¦
MWENYEKITI: Waheshimiwa naomba utulivu ndani ya ukumbi.
MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetoa maeneo, tumepanda miti, lakini pia sisi ndiyo tunaolinda ule msitu. Kwa hiyo, ninaomba Serikali, ninaomba Wizara katika mgawao wa vibali kwenye shamba la msitu wa Sao Hill lazima watu wanaozunguka msitu wapate, lazima wavunaji wadogo wadogo watizamwe, vijiji vitizamwe, makundi maalum hata under privilege kama vile akina mama wajane wapate, vikundi vya walemavu wasioona, walemavu wa ngozi, wasiosikia wapate vibali kupitia jumuiya zao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati huu namuomba Mheshimiwa Waziri na timu yake tunataka by name and by location tujue watu wa kule wangapi wamepata vibali? Hatutaki kukaa karibu na waridi tusinukie kama waridi. Leo hii tuko karibu na waridi lakini wanaonukia waridi wako Tanga, wako Mwanza wako Zanzibar. Wakati huu Mheshimiwa Waziri hatuwezi kukubaliana hata kidogo kwenye suala la vibali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na suala la vibali ukienda kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Madini, wachimbaji wadogo wanapewa ruzuku na Serikali. Mwaka jana Serikali imewapa ruzuku wachimbaji wadogo kiasi cha bilioni saba point something, mwaka huu wametengewa billion six point something. Je, kwa nini tusiwatengee pia ruzuku wavunaji wadogo ili waweze kununua mashine za kisasa. Kwa sababu zile mashine walizonazo tunazoita ding dong tunazotaka kuzipiga vita uwezo wake ni mdogo kiasi kwamba katika gogo the recovery percentage ni only 25, asilimia 75 inakuwa ni waste product. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali ije na utaratibu tutoe ruzuku kwa wavunaji wadogo waweze kununua mashine za kisasa ili kusudi hata wakivuna msitu basi tuweze kupata mazao yenye tija na siyo mabaki mengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo la vibali kuna suala la MPM zamani tukiita SPM (Kiwanda cha Karatasi cha Mgololo). Kiwanda cha karatasi kinapewa cubic meter laki mbili kwa mwaka, lakini cha kusikitisha MPM wanauziwa nusu ya bei wavunaji wetu wanauziwa cubic mita moja shiligi 28,000, MPM shilingo 14,000 lakini worse enough hawa MPM wamepewa kiwanda wazalishe karatasi, wanachofanya wanazalisha at a certain stage wanasafirisha raw material inaenda Kenya zinazalishwa karatasi tunaletewa hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hivyo tu, hata watu walioajiriwa pale kuna foreigners wako pale, wengine kazi yao wengine ni kuhesabu magogo kazi ambayo hata mtu ambaye ameishia darasa la pili anaweza kuifanya. Ninaomba Mheshimiwa Waziri na AG ningeomba upitie mkataba wa MPM kwa nini wao wanunue nusu bei, halafu watu wetu tununue kwa bei kubwa lakini pia tusinufaike na kiwanda hiki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu muda unakimbia ningependa pia kuzungumzia sekta ya utalii, tunakiri kwamba hii ndiyo sekta ambayo inaingiza mapato ya fedha za kigeni kwa wingi. Je, Tanzania Tourist Board (TTB) ambao wanawajibu wa kufanya promotion wameachwa kama watoto yatima, ukienda leo hii Kenya bajeti ya promotion na advertisement ni zaidi ya dola milioni 85, Uganda hapa ambao tunaona siyo washindani wetu wanatenga milioni nane USD, Rwanda milioni 11, sisi TTB tunaitengea chini ya milioni mbili, je, tutaweza kutangaza? Tunabaki tu kusema sisi ni wa pili kwa vivutio inatusaidia nini kuwa wa pili kama hatunufaiki na tutanufaika vipi kama hatuwekezi ? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tourism Development Levy (TDL) kulingana na sheria Ngorongoro na TANAPA wanatakiwa wawape TTB asilimia tatu kuchangia katika masuala ya promotion, lakini fedha zile zinaenda kwanza Wizarani zinaingia kwenye mambo mengine. Miaka mitatu, minne kabla ya sheria hii TTB walikuwa wanapewa 1.5 na TANAPA 0.5 na Ngorongoro ilitusaidia tukatangaza mpaka kwenye premier league, hivi leo hii tungekuwa tukiitangaza kwenye Leicester City unadhani tungekuwa tumenyanyua utalii kwa kiasi gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninaomba tunaposema utalii unachangia tuwekeze pia katika kuhakikisha kwamba tunajitangaza ipasavyo. Haiwezekani leo hii eti tumewatengea TTB wafanye ziara za maonyesho ziara tano unataka uvutie utalii! Haiwezekani hata kidogo tukatoka. Hata suala la vitanda kwamba ni 1.5 US dollar mimi nashauri tu-charge kwa asilimia kwa sababu mtu anayelaza kwa shilingi 30,000 unam-charge 1.5 USD, anayechajisha laki vivyo hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.