Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kukushukuru na kumshukuru Mwenyezi Mungu kuniwezesha kusimama jioni ya leo ili niweze kuchangia.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niungane na ripoti ya Kamati ya Bajeti maana mimi ni sehemu ya taarifa ile, hivyo naiunga mkono kwa asilimia mia moja. Naomba nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri na timu yote kwa ujumla. Baada ya pongezi hizo naomba nitoe michango kidogo kwa sababu naamini mengi yameandikwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nianze kwa kuipongeza kwa moyo wa dhati kabisa TRA kwa kazi nzuri ambayo wameifanya, hii achievements ambayo imeonekana ni ushirikiano miongoni mwao na wanaweza kufanya vizuri zaidi, naomba tuwatie moyo. Sisi Wabunge tuwe ni sehemu ya kuhimiza ulipaji wa kodi, bila kulipa kodi nchi hii haiwezi kusonga mbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukiachia mbali Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Mapato kwa maana ya Commissioner General, Wakuu wa Idara karibu wote ni Makaimu. Sasa haiwezekani, watu ambao wanafanya kazi nzuri na mpaka wanavuka malengo waendelee kukaimu hili halifai. Naiomba Serikali kwa kupitia Bodi husika hebu hawa watu ambao wamefanya kazi kwa muda mrefu kama Makaimu muwa-confirm na kama hawatoshi, muwaondoe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine la pili ambalo naomba kuchangia na hili limejitokeza bayana kwenye taarifa yetu, ni namna ya ushirikishwaji wa Bunge kwa kupitia Kamati ya Bajeti pale ambapo Mheshimiwa Waziri wa Fedha anakwenda kukutana na Mawaziri wenzake Arusha. Jambo hili halijaanza katika mwaka huu wa fedha, lilianza mwaka wa fedha 2015/2016 na ukisoma report yetu hatukuridhika na kile ambacho kilijitokeza na Waziri mwenye dhamana wa kipindi hicho, aliahidi kwamba halitajitokeza, lakini safari hii limejitokeza tena.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli usiopingika kwamba, wenzetu tunavyokutana nao kwa maana ya Mawaziri wa Fedha wa nchi nyingine, wanakwenda wakiwa wamejiandaa, wamehusisha Mabunge ya kwao kwamba baadhi ya mambo wanakwenda nayo wakisema haya ni ya kufa na kupona. Wanakwenda kuyatetea, wanajenga hoja na wanahakikisha kwamba yanapita.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukisoma katika taarifa ya Mheshimiwa Waziri, kuna msururu wa vitu vingi sana ambavyo vimepitishwa. Imekuja orodha ya nondo nyingi, unasema haya yametoka wapi? Alishauriana na akina nani? inachekesha mahali fulani unakuta kwamba, wanasema tuondoe kodi ili tuweze kulinda viwanda vya kutengeneza viberiti kwa sababu hatuna misitu ya kutosha!
Mheshimiwa Naibu Spika, hatuna viwanda, kiwanda chetu kilichokuwepo cha Moshi kimekufa, leo tunasema kwamba hatuna miti ya kutosha kwa ajili ya kukidhi viwanda vyetu, hivyo viwanda ni viwanda vipi? Ni kwa manufaa ya nani? Kwa faida ya nani? Naamini, mapendekezo ambayo yametolewa na Kamati ya Bajeti kwamba jambo hili litazamwe lisijirudie, hakika halitajirudia, maana Mheshimiwa Waziri ni msikivu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu yangu nyingine ni kuhusiana na suala zima la mradi wa maji na hasa maji vijijini pamoja na suala zima la ujenzi wa zahanati na vituo vya afya. Tumependekeza kwamba iongezeke tozo ya sh. 50/= ili jumla iwe sh. 100/= kwenye tozo za mafuta kwa maana ya petrol na diesel. Hii itatuwezesha kutupatia kiasi cha shilingi bilioni 250 na tumependekeza kwamba mgawanyo wa pesa hizi bilioni 220 iende kutatua tatizo la maji vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna Mbunge hata mmoja ambaye anaweza akaniambia kwamba kwenye Wilaya yake hawana tatizo la maji, hayupo! Kwa hiyo, ni vizuri tukatoka jasho jingi kulikoni tukasubiri kuja kuvuja damu nyingi. Naomba Mheshimiwa Waziri na Serikali kwa ujumla mlisikilize. Pia tumependekeza kwamba bilioni 30 iende kusaidia kumalizia ujenzi wa zahanati. Ni nani asiyejua kwamba ukirudi kwenye vijiji vyetu, wananchi wameitikia kwa moyo wa dhati wakajenga Zahanati zikafika usawa wa lenta, leo ukienda unamwambia mwananchi ashiriki kwenye shughuli nyingine ya maendeleo wakati maboma anayatazama hapati huduma ya afya, hawatuelewi. Kwa hiyo naomba hii shilingi bilioni 30 iende kutatua tatizo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, karibia mwisho, nimesikia Serikali wana mapendekezo kwamba safari hii wanaenda kufanya adjustment kwa inflation rate ya five per cent, ni jambo jema! Lakini jambo hili haliwezi likaenda in a blanket form, lazima kuwe na exceptions, ukiongeza kwenye bia haina tatizo kwa sababu wauzaji wa bia wameongeza bei tangu mwezi Februari, bia zimeongezeka kutoka sh. 2,300/= mpaka 2,500/=. Kwa hiyo hiki ambacho mnafanya adjustment is ok! Wala haitaathiri chochote, kwa sababu walishaanza ku-enjoy!
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo langu nalipata kwenye suala zima la vinywaji baridi na hasa soda na juisi. Hivi leo hii tunasema kwamba tunaweka excise duty ya asilimia tano kwenye soda na wakati huo Serikali hiyo inasema kwamba tunataka Mtanzania mnyonge ambaye ndiyo mnywa soda, leo hii ndiyo tunaenda kumwwekea five percent! Ukitazama kipindi hiki ndiyo kipindi ambacho wenzetu waliojaaliwa kufunga wanafunga, anataka wakati anapata futari yake apate na juisi, apate na soda. Ndiyo kipindi kweli Serikali mnataka mkaongeze hiyo? Bei ya soda haijapanda kwa ujumla kama miaka mitano, leo hii mnataka itoke sh. 500/=, iwe sh. 600/=, halikubaliki hili! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tuna vyanzo vingi, let‟s think outside the box.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.