Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza kabisa nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia leo kusimama hapa na kwa kweli nina kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa sababu hiki ni kipindi changu cha tatu ndani ya Bunge, namshukuru sana Mwenyezi Mungu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri na nimpongeze kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya na Baraza la Mawaziri. Watu wamekuwa wanafanya kazi vya kutosha, wanapiga kazi ambayo inasifika sana na kila mtu kwa kweli anaona utendaji wao, ingawa kuna wengine wamezidi zaidi, wengine viwango vyao ni vya juu sana. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuzungumzia kuhusu suala la makato ya kwenye kiinua mgongo. Hapa Mheshimiwa Waziri wa Fedha amegusa pabaya kwa Waheshimiwa Wabunge. Hata hivyo, nafahamu kwamba una busara sana, kwa hiyo utafikiria tena upya ili angalau mambo yakae vizuri sina haja ya kueleza zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza bajeti hii ni bajeti ambayo ina kila sababu ya kutuonesha na kutupa imani kwamba huko mbele tunakokwenda pako vizuri sana. Naisifu kwa sababu angalau imetuonesha na inatupa picha kwamba huko mbele yale ambayo tunayafikiria yameanza kidogo kuja.
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na suala zima la uchumi wa viwanda. Tunapozungumzia suala zima la uchumi wa viwanda, najiuliza, kwamba tunazungumza kuhusu suala la uchumi wa viwanda je, tuko tayari? Kwa sababu tunaweza tukakaa tukazungumza mambo mazuri sana na tukawa na mipango mizuri sana, tukapiga makofi hapa tukawa na sifa nyingi sana lakini tusipofunga mikanda na kusema kwamba hapa sasa tumeamua kufanya kazi vya kutosha, haya masuala yataishia kwenye makaratasi na utekelezaji wake utakuwa ni mgumu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivyo kwa sababu lipo jambo moja ambalo sijapata picha sawasawa, suala hilo ni la Inter-Ministerial Coordination. Wizara hii na Serikali hii kwa ujumla kwenye suala hili la uchumi wa viwanda, Wizara ya Kilimo inashirikiana vipi na Wizara ya Elimu, Wizara ya Nishati, Wizara ya Maji na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivyo kwa sababu tunapozungumzia uchumi wa viwanda, huu ni uchumi na ni biashara ambayo ni mkakati wa muda wa kati na muda mrefu. Sisi wengine siyo wafanyabiashara wakubwa, lakini angalau tunajaribu jaribu kidogo. Kwa hiyo, ninapozungumzia hivi ni kwa sababu tukisema kwamba tunazungumzia viwanda lazima tujiulize, Wizara ya Elimu imejiandaa kwa kiwango gani? Wizara ya Maji licha ya kwamba Tanzania ni Taifa ambalo ni la tatu duniani kwa wingi wa maji, imejiandaa kwa kiwango gani ili kuweza ku-facilitate? Kwa sababu kiwanda bila maji ni kitu ambacho hakiwezi kwenda. Wizara ya Kilimo imejiandaaje? Wizara ya Nishati imejiandaaje?
Mheshimiwa Naibu Spika, tusipokuwa makini tutajikuta kwamba watu wanakuja, wanasema sisi ni wawekezaji tunataka kuwekeza, mimi nataka kuja kuwekeza labda pengine kwa wananchi wangu wa Shinyanga kule, nataka nifungue kiwanda cha kitu fulani, lakini akikaa anaanza kwanza kujiuliza wakati anafanya due-diligence, hivi maji hapa nitayapataje? Anajiuliza hivi umeme bei yake na upo kwa kiwango gani? anajiuliza hivi kwa mfano, kama nikifanikiwa kama endapo nitawekeza kwenye kilimo, masoko yako wapi? Anajiuliza hivi, hapa nikifungua kiwanda human resource nitaitoa wapi? Kwa hiyo, haya ni maswali ambayo inatakiwa kama Serikali kwa ujumla wetu tujiulize kwa pamoja ili tuweze kuwa wote na kauli moja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivyo kwa sababu sisi kama Watanzania, wapo Watanzania ambao tunafanya kazi vizuri sana, lakini wapo watu ambao wamezoea business as usual. Wao kazi yao mtu anaingia ofisini, tunaona hata kwenye ofisi na taasisi za Serikali, mtu anaingia asubuhi saa mbili anatoka saa tisa, uvivu na ile kukaa tu kwa kujiona kwamba mimi sina tatizo lolote yaani mtu anakaa tu ile laissez-faire imekuwa ni tatizo letu. Kwa hiyo, hatuna budi sisi kama Viongozi na Wanasiasa tuseme kwamba tumejiandaa vipi kwenye hili suala.
Mheshimiwa Naibu Spika, mfano tu mdogo nitolee, National Housing ni Shirika letu la Umma, lakini siyo wawekezaji, National Housing, wanajenga nyumba za Serikali wanaziuza, Wabunge tumekuwa mara nyingi sana tunapiga kelele kwamba nyumba hizi bei yake ni kubwa sana, lakini ukikaa na National Housing wanakwambia kwamba tunapokaa wakati tunaanza hii project ya kuanza kujenga nyumba sehemu, tunajikuta kwamba maji mimi mwenyewe National Housing ndiyo nivute, umeme mimi mwenyewe ndiyo nikae nifanye hizo jitihada, kwa hiyo unajikuta ile pesa ambayo unaiweka pale ni kubwa sana kiasi ambacho baadaye inabidi irudi kwa mlaji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ambalo nataka kuzungumzia ni kuhusu suala zima la mifumo yetu pia. Mifumo yetu na system yetu ya nchi ya kuchukulia mambo, lazima tubadilishe pia sheria zetu za kazi kabla ya kuanza kukaribisha hawa wawekezaji. Sheria ya Kazi iliyopo sasa hivi inatakiwa iwe fair kwa mwajiri pamoja na mwajiriwa. Hivi sasa unakuta Sheria ya Kazi ime-base zaidi kwa yule mwajiriwa kiasi kwamba anajiona kama Mungu mtu, sasa nini kinachotokea?
Mheshimiwa Naibu Spika, kinachotokea sasa ni kwamba, watu wanafanya kazi, mtu anajua kwamba kwa mfano, mimi kama labda nafanya kazi kwenye shirika lolote labda pengine tigo, airtel na kadhalika, anaweza mwingine aka-misbehave, mwingine anafikia kiwango hata cha kuiba lakini haya mashirika na haya makampuni, hiki naomba Serikali kwa kweli tujitahidi sana, tuwe makini sana, tukae tujiulize na ikiwezekana tuunde timu ya kuangalia hawa wawekezaji tu tulionao hapa, sasa hivi kabla ya kuwakaribisha hawa wengine kwenye uchumi wa viwanda, wana matatizo gani? Maana kinachotokea sasa hivi, mtu anaiba airtel au anaiba tigo kwa mfano au anaiba sehemu nyingine yoyote lakini kinachotokea ni kwamba lile shirika au hiyo ofisi wanamchukua yule mtu wanamwambia tu naomba u-resign.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.