Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa muda na mimi nichangie. Kwanza na-declare interest mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Bajeti na nimefurahi sana kusoma hotuba ya Mheshimiwa Waziri, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wake, hotuba yake ni nzuri inajieleza vizuri sana kwa sababu imegusa maeneo muhimu yote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala ambalo limenifurahisha sana ni kwamba, hotuba ya Waziri imegusa sana malengo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi, mambo ambayo tuliahidi, Mheshimiwa Rais aliahidi na Wabunge huwa tunasema kwenye Majimbo yetu, yote yameandikwa humu. Tunakuombea sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha haya tuliyoandika Mungu atusaidie tuweze kukusanya vizuri kodi ili tuweze kutekeleza. Jambo lolote ili lifanyike vizuri lazima kuwe kuna fedha, bila fedha hatuwezi kufanya kitu chochote.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimempenda sana Mheshimiwa Waziri ameweka mikakati jinsi ya kupata hizi trilioni 29. Kupata trilioni 29 ni nyingi sana ukilinganisha na mwaka 2015/2016 tulikuwa na bajeti ya trilioni 22 sasa hivi imeongezeka tuko trilioni 29, kukusanya mpaka tufike trilioni 29 ni muziki mkubwa. Ameeleza vizuri sana kwenye hotuba yake kwamba atapataje hizo trilioni 29, nampongeza sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Bajeti, tumeeleza vizuri sana kwenye bajeti. Namwomba tu Waziri wakati anahitimisha hotuba yake hii aangalie na mapendekezo ya Kamati ya Bajeti ni ya msingi na ukiyasoma vizuri pale utakuta kuna mambo mengine tunaenda sawa, kuna mambo mengine tumetoa ushauri. Jambo ambalo limenifurahisha, tumesema kwamba Tanzania itakuwa Tanzania ya viwanda na tumesema lengo kubwa kuwa Tanzania ya viwanda ni kugusa watu wa kima cha chini. Hiyo ni kweli kabisa nami hiyo nimeipenda sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania ya Viwanda ili ikamilike vizuri kuna mambo Mheshimiwa Waziri ameeleza, amesema kwamba, atahakikisha anajenga reli ya kati kwa kiwango cha standard gauge. Tunajua ni mwaka huu wa fedha wa 2016/2017, lakini hatujui kwamba reli itakwisha kwa mwaka mmoja, tunaweza tukaanza mahali pazuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri sana katika uchukuzi, ukiangalia bajeti ya Uchukuzi na ukachukua bajeti ya Ujenzi tuki-compare pamoja inatenga trilioni nne. Hizi trilioni nne zikisimamiwa vizuri, tukaanza kujenga vizuri hiyo reli ya kati, itatusaidia sana na hii concept ya viwanda itakwenda vizuri sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, nataka nimwambie Mheshimiwa Waziri kitu kimoja, reli hizi tunazo nyingi sana. Tuna reli ya Kati, tuna TAZARA, tuna reli nyingine hii inatoka Tanga inakuja Moshi mpaka Arusha. Tunapozungumza viwanda maana yake malighafi zote tutatumia reli kwa kusafirisha mizigo yetu. Namwomba Waziri wa Fedha, tuna reli nyingine ile inayopita Makambako, kwenye Jimbo langu pale ya Mgololo, watuwekee station pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, tukiwa na station ya reli ya TAZARA pale, tunajua wasafiri au wanaosafirisha mbao badala ya kutumia barabara ya lami ambayo tunajua barabara inaharibika kila siku, basi mbao zitasafirishwa kwa njia ya treni, hapo watakuwa wametusaidia sana. Kuna kituo kidogo sana, treni pale inasimama hata dakika tano haifiki, inakuwa ni shida sana pale, namwomba Waziri alifikirie suala hili pia.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine amegusia sana kwamba, ataimarisha bandari, ni kweli tukitumia bandari zetu za Tanzania tutakuwa tumefika mahali pazuri sana. Tunayo bandari ya Dar es Salaam, tuna bandari ya Tanga, tuna bandari ya Mtwara na sasa hivi kuna bandari moja tunajadili Bandari ya Bagamoyo, tuna Bandari ile ya kule Mbamba Bay. Bandari zote hizi zikiimarishwa vizuri uchumi wa Tanzania utakuwa vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri ameongelea vizuri sana kwenye elimu, nimempenda sana. Ametenga karibu trilioni 4.7. Tukiimarisha elimu, Watanzania tukipata elimu nzuri, watoto wetu wakisoma vizuri Vyuo Vikuu tutapata wataalam wazuri sana. Ukipata wasomi wazuri hata vitu vya kugombana gombana vidogo hivi wengine wanatoka toka, wanakimbia kimbia wakielimika itakuwa haipo. Hii elimu sasa hapa naona mwaka huu Waziri wetu wa Fedha ameamua, maana kutenga trilioni 4.7 haijawahi kutokea. Kwa hiyo, ameliangalia vizuri sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulisema hatuna wataalam wa gesi. Nashauri gesi itatutoa, gesi ni kitu kizuri sana katika uchumi wa nchi, tukipata wataalam wa gesi wakatengeneza vizuri, nchi yoyote duniani yenye gesi na mafuta uchumi unakua haraka sana tuki-contol vizuri, lakini tukishindwa ku-control gesi na mafuta, basi uchumi hauwezi kukua. Kama tunataka tufikie malengo lazima tuhakikishe gesi na mafuta tume-control vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, uzalishaji kwenye viwanda wengine wamesema sasa hivi wanashindwa kutumia gesi kwa sababu ni gharama kubwa. Nadhani Waziri wa Viwanda atatusaidia, kuna viwanda vingine havitumii gesi lakini ukitaka upate production kubwa, utumie cost ndogo lazima utumie gesi. Sasa wengine wanasema gesi ni gharama, wanakimbilia kutumia umeme, suala la gesi hii nataka nisisitize sana, Tanzania lazima tujikite vizuri kwenye gesi. Gesi na mafuta ndiyo neema pekee, ndiyo tutaondokana na umaskini. Ukisema unataka kuuvua umaskini, lazima tuhakikishe kwamba pato la Taifa limekua kwa kiwango kikubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri ameeleza vizuri, amesema kwenye focus hapa kwamba mwaka 2016 pato la Taifa litafikia 7.2, hii kuipata siyo mchezo! Mwaka jana tulikuwa na point zero sasa hivi unasema point mbili, hii mbili kuipata siyo mchezo, lakini tuki-control vitu ambavyo ni vya uzalishaji tunaweza tukafikia.
Mheshimiwa Naibu Spika, tukisema maisha ya kila mtu maana yake tunaangalia hata maisha ya vijijini. Maisha ya vijijini tunaangalia nini? Tunaangalia watu wana maji? miundombinu ya maji imejengwa? Vituo vya afya tumejenga? barabara zile ambazo hazipitiki zinapitika? Zahanati zimekwisha? Vituo vya Afya vinafanya kazi? Basi tukifanya vitu vya namna hii tutafikia mahali pazuri sana. Mpaka sasa hivi kwenye bajeti, wananchi sasa wana imani kubwa sana wanasema tutapata maisha bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri umesema utafufua viwanja vya ndege. Sasa kuna sehemu nyingine hata viwanja vya ndege watu wanasema sisi hatupandi ndege tunataka barabara. Nadhani barabara zile ziwekwe kwa kiwango cha lami ambacho Serikali iliahidi, itakuwa imefanya vizuri sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa sababu ni kitu kizuri sana. Ahsante sana.