Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DUSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii ili nichangie kwenye Mpango uliowasilishwa na Serikali. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema ambaye kwa rehema zake amenipa kibali niwe miongoni mwenu kuwatumikia Watanzania kupitia Bunge hili Tukufu. Vile vile, nitumie fursa hii kuwashukuru sana ndugu zangu wa Mkinga kwa kunipa heshima kwa mara ya pili, kuwa Mbunge wao niweze kuwawakilisha katika Bunge letu ninawashukuru sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawaahidi kuwatumikia kwa uwezo wangu wote kwa maarifa ya hali ya juu, na niimani yangu kwamba, kile tunachokikusudia tutakipata. Nitumie fursa hii vilevile kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa jinsi ambavyo ameanza kushika hatamu za kuliongoza Taifa letu. Watanzania wana imani kubwa na uongozi wake, nimpe maneno ya kumu- encourage kwamba, tupo pamoja naye katika kuwatumikia Watanzania na Watanzania wanaamini kwamba, kasi ya mabadiliko waliokuja nayo itakuwa ni kasi ya ukweli. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie maneno, niazime maneno ya Rais wa 33 wa Marekani aliyekuwa akiitwa Harry Truman aliandika katika memo yake, Years of Trial and Hope katika ile volume ya pili anasema, „‟Being a President is like riding a tiger, a man has to keep on riding or be swallowed.”
Anaendelea kusema: “A President either is constantly on top of events or if he hesitate events will soon be on top of him.” Mwisho wa kunukuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kumwambia Mheshimiwa Rais Watanzania wana imani naye, aendelee na mwendo huo aliouanza nao bila ku-hesitate, tunaiona Tanzania yenye mabadiliko na mafanikio makubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo sasa nichangie mpango huu ulioko mbele yetu. Nimejaribu kuusoma mpango huu, lakini vilevile nikapata fursa ya kusoma Household Survey Report, lakini vile vile nikasoma report ile Human Development Report nikajaribu ku-combine maudhui tunayoyapata kutokana na taarifa zile. Maudhui ya taarifa zile yanatuambia kwamba tuna namba nzuri sana za mafanikio ya ukuaji wa uchumi. Namba zile zinatofautiana, ukisoma household survey na ile report nyingine zinatofautiana takwimu kidogo lakini bottom line ninachosema ni kwamba, hatujafanya vizuri sana katika maendeleo ya binadamu, maendeleo ya watu wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sisi ni viongozi lazima tuwe wakweli kwamba, tuna changamoto kubwa mbele yetu ya ku-translate ukuaji wa uchumi ili uweze kuleta maendeleo ya watu. Ndiyo maana hapa naipongeza Serikali kwa kutuletea Mpango huu wa Pili ambao una vionjo vinavyoonyesha kwamba, tunakwenda sasa kwenye kuunganisha ukuaji wa uchumi lakini vilevile ku-translate ukuaji huo kwenye maendeleo ya watu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumzia kujenga uchumi wa viwanda ambavyo vitazalisha ajira, viwanda ambavyo vitapelekea kupunguza umasikini, tunaelekea huko. Lakini lazima tujiambie kama viongozi, tuwe wakweli tujiambie kwamba mMango huu tuliouleta ambao tunaenda kuufanyia marekebisho ili baadaye uje upitishwe ndani ya Bunge hili, utekelezaji wa Mpango huo tutakaokuwa tumeuleta, ukiwa chini ya asilimia 70 tutakuwa tumeshindwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, lazima tuwe na mikakati madhubuti ya kuhakikisha hatushindwi. Takwimu zinatuambiaje, takwimu zinatuambia tulilenga kuwa na maeneo ya kilimo cha umwagiliaji hekta 1000 tumetoka kutoka kwenye hekta 345 tumekwenda kwenye hekta 461. Lakini hekta tulizonazo zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji katika nchi yetu tuna hekta milioni 29.1, tulichofanikiwa ni asilimia 0.39.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima tuje na mikakati ya kuhakikisha tunakwenda mbele. Nimeona hapo ujenzi wa viwanda, ujenzi wa bandari ya uvuvi ni jambo zuri, lakini ili tufanikiwe lazima tuunganishe jambo hili la ujenzi wa bandari ya uvuvi tuliunganishe na jambo la ufugaji wa samaki maana dunia ndiyo inapokwenda huko. Haiwezekani leo hii nusu ya samaki wanaoliwa duniani wanatokana na ufugaji wa samaki halafu sisi tusione umuhimu wa kufuga samaki, lazima tubadilike. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, bandari ile itakapojengwa lazima tujenge miundombinu ya ufugaji wa samaki, twende kisasa lazima tuwe na aquaculture industrial zone. Tuunganishe pale, bandari ya uvuvi, viwanda vya kuchakata samaki, viwanda vya kuchakata barafu na kadhalika na kadhalika na ufugaji wa samaki uwe pale pale. Katika maeneo yaliyotajwa katika kujenga bandari. Nilisema kipindi kilichopita iliainishwa bandari ya Dar es Salaam wote tunajua. Bandari ya Dar es Salaam hapafai kuna msongamano mkubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili, Moa kule Mkinga namshukuru Rais maana kila alipokuwa akisimama kutoa hotuba yake anasema ukanda wote wa bahari kutoka Moa kule Tanga mpaka Mtwara hakuna kiwanda cha samaki. Njooni pale Moa wekeni bandari ya uvuvi maana katika maeneo yaliyotajwa matatu Moa ipo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la tatu lilitajwa Bagamoyo lakini Kamati iliyopita ilitushauri hapa ndani. Ikasema hivi tunaondoaje Chuo cha Mbegani, twende tukajenge bandari ya uvuvi, ni imani yangu Serikali imesikia njooni Moa tuweke mambo vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa viwanda lazima uzingatie vile vile kuweka mkazo kwenye kujenga.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Muda wako umekwisha.
MHE. DUSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.