Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. James Kinyasi Millya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JAMES K. MILLYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nieleze masikitiko yangu makubwa kwamba wafugaji wanapambana na nini? Wanapambana na dola nyingi dhidi ya uhai wa watu. Wizara hii ni Wizara pekee yenye dola nyingi kweli ambazo interesting group, zingine ambazo ziko nje ya nchi zina-interest, na mimi hapa imebidi nitoe kidogo leo elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini tumeanza utalii nchini mwetu? Mwaka 1892 alikuja Muaustralia mmoja anaitwa Oscar Bowman, mwaka 1913 akaja mwingine anaitwa Stewart Edward White mzungu wa Kiingereza, akaja mwingine anaitwa Bernard Dimezec pamoja na mtoto wake anaitwa Michael wakaandika kitabu kimoja kinachoitwa Serengeti shall never die. Baada ya wazungu hawa kuandika vizuri kitabu hicho, Waingereza, mwaka 1959 wakaamua kuwaondoa wafugaji wa Kimasai Serengeti, wakasema wala hawafai. Tumewatunzia mazingira hayo kwa damu na jasho letu tukiwapa na ng‟ombe wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nitoe takwimu nyingine, kwa nini kuna migogoro ya wafugaji na wakulima nchi hii! Serengeti zimeondoka square kilometers 14,750 kutoka kwa wafugaji, Mkomazi - square kilometers 3,500 za wafugaji, Ngorongoro zimeondoka square kilometers 8,300 za wafugaji, Tarangire National Park zimeondoka square kilometers 2,850 za wafugaji, watu hawa mnawapeleka wapi! It’s a calculated genocide, mnataka maisha yetu yasiwepo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati huo aliyekuwa Waziri Mkuu wa nchi hii, Edward Moringe Sokoine, kati ya mwaka 1948 na 1958 ndipo wakati alikuwa anamaliza shule ya msingi na sekondari. Mikataba hii inaingiwa, mnaondoa maeneo haya makubwa kutoka kwa watu wetu. Where were there any informed consent? Naongea hivi, kuna wafugaji wako Zambia wanasuka watu nywele, kuna wafugaji wako Dar es Salaam wamekuwa walinzi, Serikali mnawaonaje, tunaanza kuwa watu wabaya kwenye nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mnatupiga, tumewahifadhia mazingira haya yote tukiamini kwamba tunatunza maisha yetu. I declare interest, siamini kwamba utalii ni mbaya, lakini utalii mbaya unaoumiza maisha yetu ni utalii usiokubalika na nitakuwa wa mwisho kukubali utalii wa namna hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wanauliza maswali mengi, wanasema mifugo inaharibu mazingira, mmoja amezungumza hapa, hivi ni ng‟ombe gani anayeua tembo, ni ng‟ombe gani anayeua simba. Lakini geuzeni swali upande wa pili, watu wanaotegemea mifugo, karibu watu milioni mbili nchi hii, geuzeni usemi kwamba hawa mifugo wamekufa, its their livelihood, leo Serikali ianze kuwalisha hawa, mnaongelea 17 percent ya GDP ya nchi. Je, mkianza kuwalisha watu hawa kwa sababu hawana mifugo, hawana maisha, itakuwa ni mbaya sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisikitika kwenye kauli ya Mheshimiwa Waziri juzi na bahati mbaya wafugaji wa Kimasai wamekupigia kura kwa takribani miaka15 kule Same. Unasema mifugo haifai, mifugo inaumwa, wanyama wasisafirishwe. Sasa nina maswali mawili; maana yake ni kwamba hawafai kuliwa na kwamba maisha ya watu ni ya bei rahisi kuliko pesa? Swali la pili, je, tuambiwe kwamba ni kauli ya Serikali kwamba wale wote wanaotegemea nyama nchi hii na wale wanaosafirisha kwenda Mataifa mengine wasisafirishe nyama kwa sababu wanaumwa, itoke kauli ya Serikali? Mheshimiwa Waziri amenisikitisha sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, kuna WMAs, tunachoomba wafugaji wa Kilindi, Mheshimiwa Msigwa ameongea hapa milioni 25, ndugu yangu naomba upate hili, tuna ng‟ombe milioni 25, hatutaki kuongezewa eneo, mipaka ambayo iliwekwa kabla sisi hatujawa na akili ya kisheria na ndiyo maana unaona Wamasai wengi, Mheshimiwa Ole-Nasha, wengine wote wanasoma sheria kwa sababu ya uonevu mkubwa. Sisi hatuli wanyamapori hao, hatuli simba, hatuli swala, tunawatunzia, lakini basi let it be fair, na ninyi msituumize. Kimotorok mnatufukuza, Emoret mnatufukua, Same mnatufukuza, Kilosa mnatufukuza, Bukombe mnatuumiza, Hanang‟ nina picha hapa, maskini wa Mungu mfugaji anatoka Katavi ameumizwa, kuna PF3 hapa. Mnatuumiza, mmetufanya watumwa kwenye nchi yetu. Naomba Serikali mkae chini mtufikirie. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaamini kwamba utalii ni kitu kizuri, lakini Waheshimiwa Wabunge iwe fair. Naomba Sheria za WMA zilianzishwa na jamii, Kifungu kile cha 12 kilichoanzisha sheria hiyo badilisheni. Tunapata hela zetu, Simanjiro tumekataa WMA, lakini Kiteto na Longido wanafanya WMA. Mheshimiwa Waziri, hela zinachelewa sana, tunaomba mtume hizi hela mapema. Lakini kile Kifungu cha 51 cha sheria hiyo, ongezeni percentage, imekuwa ni kidogo sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeumia sana, Wamasai hawajasoma nchi hii, sheria za nchi hii hazijaangalia bado watu hawa. Kule Afrika Kusini wakati wa ukombozi, mwaka 1994 wakasema tuleteni an affirmative action. Tunacholilia hapa, wengine tumesoma siyo kwa sababu ya sera za CCM, ni bahati za makanisa na bahati za wengine wazungu tu. Mmetusahau muda mrefu, mnatuumiza muda mrefu, naombeni mfikirie kwamba Bunge hili lianze kutenda haki kwa ajili ya watu hawa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, fikirieni mifugo, its not about business, it is a livelihood. Mimi nisipokuwa na ng‟ombe siangalii kuhusu hela. Lakini lingine ni lile linahusiana na Mheshimiwa Lowassa na Mheshimiwa Sumaye, Wakili mwenzangu ameongea, ninasikitika sana, watu hawa wanasahau records. Mwaka 2006 Lowassa akiwa Waziri Mkuu wa CCM alifukuza mifugo Ihefu, hapakuwa hata siku moja na tamko la Kiserikali kutoka kwa Lowassa na Sumaye kutapanya mifugo yote nchi hii, msipotoshe umma. Nimuombe Wakili mwenzangu anapoanza kusimama aongee na authority, tunatetea utu, hatutetei biashara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, Mungu awabariki sana. Ahsante sana.