Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ninaomba dakika zangu kumi, kila nikichangia ninapewa dakika mbili, dakika tano wakati wengine wametumia dakika kumi; naomba unitendee haki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nimpe tu pole Mbunge wangu Mheshimiwab Issaay, inatia hasira wakati mwingine lakini pole sana kaka yangu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze tu kwa kusema, ni kweli kwamba sekta ya utalii inatoa mchango wa asilimia 25 ya pato la fedha za nje katika nchi yetu, lakini ni kweli wakati mwingine inakuwa inaumiza baada ya kuona kwamba uharibifu mkubwa unafanywa na wanyama... Wabunge naomba tusikilizane.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uharibifu mkubwa unafanywa na wanyama, lakini badala yake fidia ama kifuta jasho kinachotolewa ni kweli kwamba ni kidogo sana. Hii ndiyo inayopelekea kwa kweli watu kupata shida wakati wa kampeni za uchaguzi baada ya kuona kwamba hawatendewi haki. Inafika mahali labda wanyama wanaonekana wa thamani kuliko mwanadamu. Ni kweli kwamba hili linapaswa kuangaliwa kwa umakini sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia niseme kwa upande wa Wilaya ya Babati Vijijini, wanyama walifanya uharibifu na Mheshimiwa Jitu Soni kwa zaidi ya miaka mitano amekuwa akifuatilia kifuta jasho cha wananchi husika, lakini katika pesa ambazo zinafikia zaidi ya shilingi milioni 100 ameambulia kupata shilingi milioni 12, tunaomba Wizara hii sasa iweze kuangalia namna gani hawa wananchi walioathirika wanaweza kupata fidia hiyo japo kidogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nitoe shukrani za dhati kwa TANAPA kwa kuweza kufungua geti la Sangaiwe pamoja na geti la Mamire ili kuweza kuruhusu wananchi kufanya biashara zao ndogo ndogo. Niombe Wizara iweze kutusaidi kukusanya hiyo 0.3 levy ili kwamba mapato haya yaweze kuwa ya msaada kuliko inavyofanyika sasa, maana hoteli zinazozunguka hifadhi hizo zimekataa kata kata kulipa tozo hizo za 0.3 percent.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati huo huo naomba pia niseme miaka michache iliyopoita wakati wa Operation Tokomeza mama mmoja kule katika Kata ya Galapo, Mkoani Manyara aliauwa, ikaundwa Tume ya Kijaji mpaka sasa hatujapata jibu lolote kuhusu mauaji yale. Tunaomba Wizara itusaidie kujua nini kiliendelea kuhusu mauaji yale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na zaidi sana naomba ni-declare interest kwamba mimi pia ni mdau wa utalii. Kuna utitiri mkubwa wa kodi zisizopungua 15 katika uwekezaji huu wa utalii. Haiwezekani wananchi wetu wakalifikia goli la kuondokana na umaskini wakati kodi ni nyingi kupita kiasi. Mheshimiwa Mchengelwa ametoka kuzungumza habari ya night bed levy.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sijui ni nini maana ya mtalii. Inawezekana mtu akitoka Arusha kwenda Dar es Salaam kwenda kumuuguza mgonjwa wake Muhimbili na akawa analala kwenye hoteli pale Dar es Salaam anaweza akawa anaitwa mtalii. Tatizo ni kwamba kodi hii haiko-fair. Kama ni Mount Meru Hotel inalipa one point…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kodi hii ya night bed levy kwa kweli imekuwa kikwazo kwa wafanyabiashara wadogo. Unakuta mtu hoteli yake anauza vyumba kwa shilingi 30,000 au 50,000 analipa the same amount na mtu ambaye ana hoteli ya kitalii, au let us say hoteli ya Mount Meru ama hoteli nyingine kubwa za nyota nne au nyota tano. Sasa usawa uko wapi? Hili litazamwe na Wizara hii, Mheshimiwa Maghembe tunaomba ulitupie jicho, night bed levy imekuwa kikwazo kwa wafanyabiashara wadogo kama wale wenye guest houses wanatozwa kodi kwa nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini wakati huo huo niseme pia TALA license imekuwa ni kilio cha muda mrefu. Hapo Kenya wanatoza dola 300 kwa TALA license, lakini pia wanatoza kwa gari hawatozi kwa kampuni. Huku kwetu una gari moja, tano, mbili, mia tano unatozwa dola 2,000 kwa nini? Hili kimekuwa kilio kikubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kulipia TALA license unalipa land rent, unalipa tax zote 15, huyu mtu anapataje faida? Anawezaje kutusaidia kuongeza ajira kwa vijana wetu? Nilisema tena watu wengi wameweka magari yao nyumbani, wameshindwa kufanya biashara ya utalii kwa ajili ya utitiri wa kodi. Ifanyike review kwenye kodi hizi ili utalii wetu uweze kuleta tija katika nchi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niseme tu, inawezekana sana kuhakikisha kwamba pia na misitu yetu inatusaidia. Ukienda nchi za watu watoto wanagombana na wazazi wao kubadilisha ipad, laptop mpya, smart phones, sisi tunajadili habari ya dawati wakati misitu iko hapo. TFS wanakusanya zaidi ya shilingi bilioni 50, ni ukataji wa miti tu unaendelea, hakuna miti inayorudishwa kupandwa. Tutakwenda hivi mpaka lini? Mtoto kukaa kwenye dawati Tanzania inakuwa ni privilege, kweli? Tutaondoka lini huko?
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilikuwa nafikiri kwamba tunaweza kurekebisha hali hii, kama tuna sera mbovu basi tuziangalie tena, tuzirekebishe ili kwamba yote yanayoendelea katika nchi hii yawe ni kwa maslahi ya Mtanzania maskini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme haraka haraka juu ya Mlima Hanang. Mlima ule ni wa tatu kwa urefu hapa Tanzania, lakini kuna uharibifu mkubwa wa mazingira unaoendelea katika Mlima Hanang. Tunaomba ikiwezekana mlima huu ukabidhiwe kwa TANAPA ili waweze kuulinda maana uharibifu unaofanyika pale ni mkubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nisiendelee sana, niwaachie na wenzangu wengine dakika chache zilizobaki.
Mheshimiwa Mwenyekiiti, nakushukuru sana na ninaunga mkono hoja.