Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wa Njombe na hasa Halmashauri ya Mji wa Njombe kumekuwa na changamoto nyingi sana kuhusiana na ardhi pamoja na nyumba. Changamoto ya kwanza ni upimaji wa ardhi. Maafisa Ardhi wamekuwa wakimilikisha viwanja kwa zaidi ya mteja mmoja. Maafisa wamekuwa wakipima viwanja ambavyo ni ndani ya mita 60 na mwisho wa siku wamejikuta wanawekewa alama ya “X” kwenye nyumba hizo na hatimaye kuwatia hofu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wamekuwa wakichukuliwa ardhi bila kujadiliana na wenye maeneo husika. Mfano, Mtaa wa Kambarage na Mji Mwema, hadi sasa hivi kuna mgogoro unaoendelea kati ya mwekezaji na wananchi. Naitaka Serikali ifanye maelewano na wenye ardhi kabla ya kuchukua ardhi hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua kutoka kwa Waziri wa Ardhi; je, mashamba, majengo na rasilimali nyingine za Njodeko na Njoruma anamiliki nani? Kwa sababu mashirika hayo yalianzishwa na wananchi ili kuleta maendeleo katika Mkoa wa Njombe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua nini kinaendelea kwenye maeneo ya utafiti Igeli na Ichenga yaliyokuwa kwa ajili ya kuwasaidia vijana? Naiomba Serikali kuona namna ya kutumia maeneo hayo kwa ajili ya vijana kujifunza na hatimaye kuwa wakulima wa kisasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali watendaji walikuwa wanakusanya kodi za majengo, asilimia 80 ilikuwa inakwenda Halmashauri na asilimia 20 ilikuwa inarudi kwenye Serikali za Mitaa. Baadaye utaratibu umebadilika, wameweka mawakala ambao wamekuwa wakikusanya asilimia 60 kwenda Halmashauri, asilimia 20 wanachukua mawakala, asilimia 20 inarudi kwenye Serikali za Mitaa. Tunapoteza mapato hayo. Nashauri Serikali kuwa kodi hizo zikusanywe na watendaji kusudi asilimia 70 iende Halmashauri, asilimia 30 irudi kwenye Serikali za Mitaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya ujenzi ndani ya mita 60, napenda kuishauri Serikali kwa Mkoa wa Njombe wawekewe utaratibu wa mita 30 badala ya 60.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha hoja.