Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja asilimia mia. Uendelezwaji wa Mji wa Kigamboni uendelee kwa kuwa Serikali imeshaanza ujenzi wa Daraja la Nyerere basi na mji ule uendelezwe ili kuleta faida ya lile daraja.
Kuhusu ujenzi wa majumba mapya (NHC) na kuyauza yaliyopo katikati ya mji uangaliwe. Ardhi ikishatumika basi, sasa mwaka 2016 tunauza ardhi, je, kizazi cha miaka 50 ijayo watajenga wapi? Nashauri tukodishe tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Upimaji Viwanja Kiholela. Serikali imeshindwa nini sasa viwanja vinapimwa hovyo na watu kisha wananchi wanadai huduma muhimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanja vipya vinapimwa lakini mradi wa viwanja 20,000 mpaka sasa watu wamewekeza viwanja vimekuwa mapori hakuna uendelezwaji. Mfano Toangoma, Kisota, Gezaulole na Somangira – Temeke, Serikali inasema nini? Gharama kubwa za rent za nyumba za NHC wakati nyumba hazina ukarabati, maji yamekatwa, umeme wa mashaka lakini rent shilingi 320,000 mpaka 280,000. Hizi sio fedha ndogo kwa mtumishi wa kima cha chini vijana wetu wanashindwa kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, gharama za kununua nyumba ni kubwa sana na nyumba ni ndogo sana huku familia nyingi zikiwa ni kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja asilimia mia.