Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DKT. NORMAN A. S. KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Waziri Lukuvi na Naibu Waziri Angeline Mabula pamoja na wasaidizi wake wote kwa kazi nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi nzuri, Hifadhi ya Kitulo imechukua hata eneo ambalo kimsingi halitumiki kwa utalii wa maua. Kwa hiyo hifadhi imepora eneo ambalo ndilo tegemeo kwa kilimo cha wananchi wa Tarafa za Matamba, Ikuwo, Lupalilo na Magoma, hasa kata zifuatazo Mfumati, Itumbu, Kigala, Ipelele, Mlomwe na Kitulo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Waziri ashirikiane na Waziri mwenye dhamana ya Utalii kurekebisha mipaka ya Hifadhi ya Kitulo ili kuondoa malalamiko ya wananchi na kuwasaidia kuendeleza mashamba yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vizuri ifahamike kuwa ulinzi wa Hifadhi ya Kitulo unategemea wananchi hawa. Ni muhimu wailinde huku wakiwa na eneo lao kwa ajili ya kulima. Mheshimiwa Waziri alishughulikie jambo hilo hasa miezi ya kuanzia Juni mpaka Septemba wakati wa kiangazi. Nawasilisha.