Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa uwasilishaji na mikakati mizuri inayomkomboa Mtanzania wa hali ya chini. Niombe mambo machache.
Mheshimiwa Mwenyekiti, gharama za upimaji ardhi zipungue zaidi ili kumuwezesha mwananchi kuweza kumiliki ardhi. Niiombe Serikali itusaidie kupima ardhi ya maeneo yaliyo pembezoni ya Singida Mjini, karibu kata nane, mfano, Mwankoko, Uhamaka, Kisaki na kwingine ili kuwezesha mwananchi kukoposheka na kuinua uchumi wa maeneo hayo, hali hii itatusaidia kuwa na mpango mzuri wa ujenzi na makazi.