Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kitabu cha hotuba ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ukurasa wa 31 – 32 amezungumzia jukumu la kuanzisha na kusimamia Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya kwa lengo la kutatua migogoro ya ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Bajeti ya Wizara ya mwaka 2011/2012 Bunge lilipitisha matumizi ya kuanzisha Mabaraza matano ya Ardhi na nyumba ya Wilaya na Tunduru ikiwa ni mojawapo. Hadi sasa Halmashauri imetoa jengo miongoni mwa majengo ya Idara ya Ujenzi na samani japo chache ili angalau Baraza lianze kufanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Waziri anapohitimisha michango mbalimbali ya Wabunge naomba mambo yafuatayo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iajiri Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi la Wilaya ya Tunduru kwa sababu kwa sasa mwenyekiti wa Baraza la Ardhi la Songea Mheshimiwa Norbet Ndimbo ndiye anayetembelea Baraza la Tunduru kila baada ya mwezi mmoja na mara nyingine baada ya miezi miwili. Hili halileti tija kwa wananchi wa Tunduru.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iajiri watumishi na wahudumu wa baraza; kwa sasa kuna mtumishi mmoja tu Bi Vumilia Chipasura, anafanya kazi kama kibarua, hajaajiriwa na anafanya kazi zote za uhudumu, ukarani na uchapaji, ikiwezekana hata huyo aajiriwe.
(c) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ijenge jengo la kudumu kwa ajili ya Baraza la Ardhi badala ya kuazima jengo Halmashauri, hii iendane na ununuzi wa samani za ofisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kuwa si vizuri kuendelea kuanzisha mabaraza mengine ya ardhi na nyumba ya Wilaya ikiwa haya yaliyopitishwa na Bunge hayajakamilika.