Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naanza kuchangia hotuba hii kwa kumshukuru Mungu aliyeniwezesha kuwa miongoni mwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nachukua fursa hii kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Tumbatu, kwa kunichagua kwa kura nyingi kuwa Mbunge wao, natambua imani kubwa waliyonayo kwangu na naahidi kuwatumikia kwa nguvu zangu zote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, napenda kumpongeza Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Magufuli kwa kuonesha imani na uwezo mkubwa wa kuiongoza nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, napenda kumpongeza Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa pamoja na Baraza lote la Mawaziri kwa kuonesha umahiri wa kuongoza katika Wizara zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuchangia hotuba hii napenda kuchangia katika maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu udhibiti wa migogoro ya ardhi nchini yanaongezeka siku hadi siku. Hii inasababishwa pamoja na mambo mengine, uhaba wa ardhi inayosababishwa na ongezeko la watu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la ongezeko la watu namshauri Mheshimiwa Waziri achukue hatua ya kushirikiana na Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani kuangalia kwa makini uingiaji wa wakimbizi ambao nao pia wanasababisha ongezeko la watu nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, teknolojia ya habari katika kitabu cha hotuba ya Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 27 (36) amezungumzia juu ya teknolojia hii, ni teknolojia inayohitaji ujuzi mkubwa. Ushauri wangu ni kwamba kazi hii pamoja na kupewa makandarasi, Wizara ichukue juhudi za makusudi kuwaelimisha wafanyakazi wazalendo ili kwa baadae kuepuka na hasara za kuwapa kazi makandarasi badala yake kazi hizo zifanywe na wafanyakazi wa Wizara hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mipaka ya Kimataifa, katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 34 (46) Waziri ameelekeza namna ya juhudi inayochukua juu suala hili la mipaka ya Kimataifa. Mheshimiwa Waziri ameeleza kukwama kwa upimaji wa mipaka kati ya Tanzania na Burundi. Namuomba Mheshimiwa Waziri anieleze ni kiasi gani kazi hiyo imeathiri zoezi hili kutokana na hali aliyoieleza kuwa ni ya kisiasa.
Mheshimwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.