Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri kukosa mamlaka ya moja kwa moja kuyawajibisha Mabaraza ya Ardhi imekuwa kero na kufanya wananchi kudhulumiwa haki zao na Mabaraza haya kwa sababu ya rushwa na uonevu mwingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali kupitia Wizara hii iangalie upya sheria iliyounda Mabaraza haya ikiwemo na namna ya kuyawajibisha ili wanaojiona miungu watu wanaoweza kufanya chochote badala ya kupunguza migogoro badala yake wameongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu migogoro ya ardhi katika kitabu sijaona Ukerewe kama sehemu inayokabiliwa na migogoro ya ardhi, hivyo naomba Wizara itambue kuwa Ukerewe kuna migogoro kadhaa ya ardhi ikijumuisha ifuatayo:-
Mpaka wa kijiji cha Nampisi na majirani zake, kijiji cha Muriti vs kijiji cha Kitangaza, mipaka katika vijiji vya Buzegwe vs Murutanga, kijiji cha Bulamba Vs Musozi, kijiji cha Bukindo vs Kagunguli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, fidia ya maeneo yaliyotwaliwa ya vijiji vya Bugegwe, Kakerege, Nyamagana, Selema, Kasulu - Nakoza itolewe.