Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na matatizo makubwa nchini juu ya ulipaji wa fidia kwa wananchi pale Serikali inapotoa/kuchukua ardhi kwa maendeleo na kuwa kero kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo mengi ya jeshi yamekuwa na migogoro kwa jeshi kutokuwa na hati za ardhi zao na wao kusema wamevamiwa na wananchi. Nashauri majeshi yote Polisi, Magereza na JWTZ wapewe hati miliki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Nyumba (NHC); nashauri mikataba yote ya nyumba iliyoingiwa na NHC na wawekezaji wengine ikaguliwe upya. Wasiwasi wangu imekabidhiwa kwa mkataba wa muda mrefu na kwa gharama kubwa mpaka Serikali itakapopata faida itakuwa ni miaka mingi.
Kuhusu maeneo ya wazi, Wizara ikague na kuwanyang‟anya wale wote waliopewa maeneo ya wazi na kuyarudisha kwa wananchi. Maeneo mengi ya michezo na kupumzika yametekwa na waporaji wachache.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upimaji wa ardhi. Halmashauri nyingi zimekuwa zinatoa tender kwa wadau kuweza kupima viwanja, nadhani ni kuiibia Serikali mapato yake na kuongeza gharama kwa wananchi. Ninachoomba Wizara ipewe pesa ya kutosha kuweza kusaidia huduma hii kuendelea na kufanya kazi zake kwa urahisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ofisi za kanda; kumekuwa na migogoro mingi ya ardhi katika mikoa hasa ya wakulima na wafugaji na maeneo ya vijijini mfano Kijiji cha Mpuguso, Wilaya ya Rungwe, wamenyang‟anywa ardhi yao ya kijiji na kujenga zahanati huku wakiwa na hukumu ya halali lakini bado wako kwenye usumbufu. Hivyo, naomba wahusika hasa ofisi ya kanda ifanye kazi yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara iwe makini kwa hati zinazotolewa kwa wawekezaji ambao wengi wanaingia na gear ya kuoa Watanzania ili waweze kupata ardhi. Kwa kushirikiana na Uhamiaji Wizara inaweza kuwabaini wawekezaji hao.