Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa heshima napenda kukushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi nichangie mchango wangu katika Wizara hii. Nimepitia kitabu cha bajeti katika kusoma nimeona uendelezaji wa miji sijaona Mji wa Tunduma. Kila mmoja anajua kuwa Mji wa Tunduma unakua kwa kasi kubwa na ni lango kuu la kuingilia nchi za Kusini na kati mwa Afrika. Hivyo, kutokuweka Mji wa Tunduma katika miji itakayoendelezwa ni kutokuitendea haki Halmashauri ya Mji wa Tunduma. Kasi ya ujenzi katika Mji wa Tunduma ni kubwa sana na hatuna kiwanja hata kimoja kilichopimwa hivyo sasa ujenzi ni holela. Pamoja na kutokuona Mji wa Tunduma katika kitabu cha bajeti, naomba Waziri atuingize.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika miaka mawili iliyopita tulifanya mchakato wa kutafuta namna ya kukopa katika taasisi za fedha na baadaye turejeshe baada ya kuuza viwanja, lakini tulikataliwa na TAMISEMI. Hivyo, tunaomba Wizara itusaidie kupata fedha katika taasisi za fedha ili kupima haraka Mji wa Tunduma kabla haujaharibika sehemu zote. Wananchi wanahitaji viwanja, hata leo ukipima viwanja 5,000 ndani ya miezi miwili hutapata kiwanja watakuwa wamemaliza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunaomba sana Wizara itupatie pesa ili tupate master plan ya Mji wa Tunduma ili kurahisisha kazi za upangaji wa mji wetu wa Tunduma. Nashauri Halmashauri zote nchini zipate master plan katika kurahisisha kupima na kupanga miji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua mpango wa kurasimisha makazi (MKURABITA). Mwaka 2012-2013 walikuja Tunduma na kupima baadhi ya maeneo kama Kata ya Maporomoko na Kaloleni katika mitaa ya Kaloleni, Danida, Kastamu, Nelo, Migombani na wakawahamasisha wananchi kufungua akaunti wakaanza kukusanya pesa na kuziweka katika akaunti ile mpaka leo hakuna kinachoendelea pamoja na kuchimba mawe yaani kuweka alama ya kuwa eneo limepimwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini mpango huu uliowaacha njia panda wananchi wa kata hizo bila kujua nini kitaendelea utamalizika?
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mji wa Tunduma kuna migogoro ya ardhi kati ya wananchi wenye mashamba na Halmashauri baada ya Afisa wa Ardhi Mteule wakati bado tuko Mbozi kupima maeneo ya watu bila kuzungumza nao na bila kuwalipa fidia na kuwauzia wananchi wengine katika Kata za Mpemba, Katete, Chapwa na Chipaka huo ulikuwa mwaka 2011 na 2012. Hivyo tunaomba pia Waziri afike katika Halmashauri yetu awasaidie wananchi kwani wanamsubiri kwa hamu kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia mpaka wa Tanzania na Zambia ni tatizo. Nyumba zimeingiliana, Watanzania wameingia Zambia na Wazambia wameingia Tanzania hivyo kuzua sintofahamu kwa wananchi wetu pamoja na Zambia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.