Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza sina budi kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya ya kutumbua majipu, kwa hilo hongera sana. Pia naomba kuendelea kumpongeza Mheshimiwa Spika kwa kazi nzuri anayoifanya na kuliongoza Bunge vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda niishauri Wizara hii ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwamba zile za nyumba za National Housing Corporation zilizopo Dar es Salaam ambazo zinakodishwa kwa shilingi 370,000 kwa mwezi kwa kweli bei hiyo ni kubwa mno ukilinganisha na kipato cha wananchi kilivyo. Walio wengi hawamiliki fedha hizo na wakati mwingine nyumba hiyo ikiharibika unaambiwa fedha hakuna, inakubidi utekeleze mwenyewe kazi ya matengenezo au upakaji wa rangi. Kwa hiyo, naiomba Wizara hii ipunguze kiwango hicho ili wananchi walio wengi wafaidike asimilia mia.