Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, napongeza utendaji wa Wizara kwa kazi inayoendelea kutendeka. Nkasi Kusini kuna vijiji kadhaa ambavyo vinadaiwa na Lwanfi Game Reserve kuwa viko ndani ya reserve yake, vijiji hivi vilikuwepo kabla ya hata reserve kuanzishwa. Vijiji hivi ni kama ifuatavyo:-
(i) Kijiji cha Kasapa, Kata ya Sintali;
(ii) Kijiji cha King‟ombe, Kata ya Kala;
(iii) Kijiji cha Mlalambo, Kata ya Kala;
(iv) Kijiji cha Ng‟undwe, Kata ya Wapembe; na
(v) Kijiji cha Namansi, Kata ya Ninde.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vipo vijiji pia vimepakana na Lwanfi na kuna migogoro ya hapa na pale kama vile kijiji cha Nkata na kijiji cha China, Kata ya Kate. Kwa msingi huo, naomba Waziri achukulie hii ni migogoro na sijaiona ndani ya kitabu chake cha migogoro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ninalopenda kuchangia ni kuhusu mashamba ya wawekezaji. Mipaka ya mashamba ya wawekezaji wawili Jimboni Nkasi Kusini ina migogoro na wananchi wanaozunguka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mashamba hayo yanamilikiwa kihalali lakini kutokana uhaba wa ardhi wananchi wanakosa ardhi ya kutosha kulima. Mashamba hayo ni yale ya Nkundi na China. Ni mashamba makubwa, Serikali ione namna ya kuzungumza na wawekezaji hawa ili kuwaachia wananchi sehemu za mashamba hayo kutokana na uhaba wa ardhi walionao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ranchi ya Kalambo inapakana na vijiji vya Nkana, Sintali, Mkomanchindo na Kasapa, pamoja na sera ya kugawa vitalu kwa waliobinafsishiwa, vitalu havitumiki vizuri na wananchi hawana ardhi. Nashauri ardhi hii igawiwe kwa wananchi kwa sababu hawana ardhi katika vijiji nilivyovitaja, hii ni muhimu sana.