Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri na kwa kazi anayoifanya kwenye Wizara yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza naomba kumshukuru Waziri kwa kunipa Baraza la Ardhi la Wilaya ya Kiteto. Tumekuwa na migogoro mingi kwa muda mrefu Kiteto lakini sasa ameshatupa Baraza la Ardhi, tunakushukuru sana na tunakupongeza sana. Tunakuomba meza na vifaa vingine vya ofisini halafu uje ulifungue lianze kuchapa kazi, hilo ni jambo la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Ardhi wamefanya kazi kubwa sana. Mpaka leo Kiteto hali ya amani inayoendelea ni kwa sababu waliweza kupima baadhi ya vijiji, mipaka ikabainishwa na watu wakaweza kuishi kwa amani kwa kipindi hiki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi iliyobaki Kiteto si kubwa sana. Namuomba Waziri aje na wataalam wake atusaidie kupima ardhi yote ili finally migogoro yote iweze kufika mwisho. Wafugaji wapate pa kukaa, wakulima wapate pa kukaa, kila mtu ajue kipande chake cha ardhi, mwisho wa siku itapunguza muingiliano ambao kwa sasa umekuwa unatuletea migongano ya kila wakati. Najua ni gharama kubwa, lakini kwa mazingira na hali iliyojitokeza kiteto tunaomba tupewe priority ili tusirudi huko tulikokwishatoka, hilo ni jambo la tatu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ile Tume ya Waziri Mkuu ya Askofu Mhagachi, ilifanya kazi Kiteto ikamaliza, ripoti imekaa. Tunaomba mumshauri Waziri Mkuu ile ripoti ije, Waziri Mkuu afike, tumalize ule mgogoro, watu wajue nini kilitokea katika ripoti ile na hatimaye watu waweze kujua wapi wanatakiwa wasimamie na nini kifanyike kwa watu wote na atakayeyasababisha matukio mengine basi aweze kushughulikiwa kulingana na ile document itakavyokuwa inaeleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Kiteto kuna NGOs nyingi ambazo zinanitia mashaka. Siku nyingine tutakuja kukuta Tanzania ilishauzwa hatujui na hivi vibali vinatolewa Serikalini. Kwa kweli NGOs ni nyingi, unashtukia NGO imezaliwa asubuhi watu wanafukuzwa asubuhi wanasema ni CBOs, jioni ni WMAs na hifadhi, sasa tumeshindwa kuelewa kipi ni kipi. Watu wameshalima mashamba, wamejenga, ni vijiji asubuhi wanakuambia hii ni hifadhi au ni WMA, hawa watu tutawapeleka wapi? Asubuhi watu wanaanza kushikiana mikuki na mapanga. Haya siyahitaji Kiteto, naomba Waziri aje hizo NGOs nyingine azipunguze, zifutwe na zijulikane zinafanya nini. Kwa sababu NGOs hizi zinafanya chokochoko za chini na ndizo zinazoibua migogoro ya wakulima na wafugaji Kiteto na kupelekea watu kupigana wakaisha. Tunaomba zifanyiwe kazi zile ambazo hazifanyi kazi vizuri zifutwe na zile zinazofanya kazi vizuri basi ziendelee na ziratibiwe kwa nini zinafanya kazi hizo na vyanzo vyao vya mapato vinatoka wapi ili tuweze kujua hawa watu wanakwendaje na wanatoka wapi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni hati miliki za kimila. Tunataka tujue, hizi hati miliki za kimila wananchi wetu wamepewa, wanajua mipaka ya maeneo na ni title, benki haziwakopeshi watu hawa, hazizikubali hizi title. Tunaomba Waziri mwenye dhamana azibane benki zinazokataa hizi title, azidhibiti, iende Serikalini, itungwe sheria, wasipewe vibali vya kufungua matawi mengine kama wanakataa hizi title. Tunahitaji watu wetu wapewe mikopo kutokana na title walizonazo kwa sababu ardhi ni yao, wana hati miliki kwa nini wasipewe mikopo kwa kutumia hizo documents zao kwa sababu wana haki nazo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshukuru Waziri amejitahidi katika kunyang‟anya watu ardhi ambao hawaitumii, kutatua migogoro kwenye maeneo mbalimbali, kwa kweli Mheshimiwa Waziri Lukuvi amethubutu lakini naomba niishauri Serikali, Mheshimiwa Lukuvi apewe ulinzi. Akienda na kasi hii Mheshimiwa Lukuvi watampiga mshale, haki ya Mungu, mshale hauna leseni, mshale haulipiwi kodi, anaweza kutembea huko maporini Kiteto na sehemu nyingine ambako watu wana hasira wakampiga mshale kwa sababu anachapa kazi, hongera sana, amethubutu kufanya hayo. Tuombe Mawaziri na viongozi wengine na Wabunge hebu tumuunge mkono Mheshimiwa Lukuvi, tumsaidie kumtatulia migogoro na sisi, kule tuliko na sisi tufanye, tusiwe ni part ya complain. Viongozi wengi wanalalamika sana, tuko kwa wananchi, migogoro mingine inamalizwa na Wabunge. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kiteto leo iko stable kwa sababu niko pale, hata kama kuna differences zozote zile lazima iwe stable, lazima itulie, wameniamini lazima watii kwa mamlaka na sheria za nchi. Wabunge twende kwa wananchi tukachape kazi, migogoro mingine ni differences tu za makabila, tabaka, uchumi, tumezidiana, amelima pakubwa, amelima padogo, ana ng‟ombe wengi, unakaa chini, mnavuta tumbaku, mnakunywa pombe, msivute ile sigara nyingine kubwa, tatua migogoro ya wananchi kabla haijaenda kwa Waziri, kabla haijaenda kwa Mkuu wa Mkoa, kabla haijaenda huko juu kwa Waziri Mkuu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuzungumzia National Housing. Nashukuru sana kuna mchangiaji mmoja amesema National Housing ina kodi kubwa, ina vitu vingi inavyolipa lakini naomba ni-create awareness, National Housing kuna siku moja inaweza kuanguka, ikashindwa kulipa mikopo. Tuwapongeze wamechapa kazi, lakini naomba ni-create awareness kwa Serikali, Marekani iliwahi kuanguka benki zikatingishika ika-shake mpaka dunia nzima na Afrika tukapata shida. Napenda kuwaambia leo wana-flow ya mikopo mikubwa, wana hizi riba na kodi wanazotakiwa kulipa, nimshukuru Waziri mwenye dhamana alishaona na amewasimamisha kuendelea na development, wajenge hizo walizonazo wakae chini, wa-plan upya kwa maana kwamba watengeneze vision wakijua kabisa kwamba wana mikopo ya kulipa, waone capability yao ya kuilipa bila baadae kuja kuitegemea Serikali na kuwa mzigo. Mheshimiwa Lukuvi naomba ulisimamie hilo na uliangalie sana kwa sababu inaweza kutokea ukawa mzigo kwa Serikali, leo ni safi, kesho shimo. Naomba muangalie sana kwa sababu wana amana za mabenki wanaweza kusababisha yakaanguka, huo ni ushauri mmoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine naomba nishauri Mheshimiwa Waziri, migogoro mingi ya ardhi imekuwepo lakini tukubaliane kwamba katika maeneo mengi watendaji wa Serikali wanaolipwa mishahara, Maafisa Ardhi wanahamisha beacon. Kiteto watu wamekwisha kwa sababu wali-divert beacons za hifadhi wakasababisha watu kuendelea kugombana. Maeneo ya wakulima yakasogea ndani watu wakaanza kupambana, huyu anasema ni hifadhi huyu anasema ni mashamba, mwisho wa siku watu wakamalizana. Hawa Maafisa Ardhi wako wahuni tunaomba uwaondoe wakae pembeni, ajiri vijana wapya, wako mtaani wana vyeti kwapani, tunaomba uwasaidie hao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naomba nishukuru, nimuombe Mheshimiwa Angeline Mabula, Naibu Waziri, amsaidie Mheshimiwa Lukuvi, kwa kazi namjua akiwa Muleba alikuwa anachapa kazi, kulikuwa na migogoro mingi Kagoma alisimama kidete akaeleza ukweli hadharani wananchi wanakukumbuka sasa chapa kazi kwa Tanzania nzima. Pia kuna Dkt. Yamungu, Katibu Mkuu wa Wizara, ni mchapakazi, chini yake kuna Makamishna tunawapongeza, chapa kazi nchi isonge mbele migogoro ipungue hapa nchini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kushukuru na kuwasilisha, naunga mkono hoja.