Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii ili na mimi nichangie Mpango uliowasilishwa na Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetujalia sote hapa tumeamka salama na tunaendelea na shughuli zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika namna ya kipekee kabisa niwashukuru wapiga kura wa Mafia kwa kuniwezesha kuwa Mbunge kwa kura nyingi sana na leo nimesimama kwa mara ya kwanza katika Bunge lako Tukufu nikichangia Mpango huu. Ninachotaka kuwaambia wananchi wa Mafia, imani huzaaa imani. Wamenipa imani na mimi nitawarejeshea imani. Ahadi yangu kwao, nitawapa utumishi uliotukuka uliopakwa na weledi wa hali ya juu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wao wenyewe watakuwa mashahidi, wameshaanza kuona baadhi ya ahadi ambazo niliziweka kwao zimeanza kutekelezeka. Wananchi wa vijiji vya Juwani na Chole wa visiwa vidogo ambavyo hawakuwa na maji kwa muda mrefu, maji yameshaanza kutoka kule. Wananchi wa visiwa vidogo vya Bwejuu na Jibondo maji wataanza kupata baada ya wiki mbili kutoka sasa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Serikali makini na Serikali sikivu ya CCM kwa kuanza na sisi wananchi wa Mafia. Nimeongea na Waziri makini kabisa Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi tukiomba watupatie meli ya MV Dar es Salaam ili kuondoa kero ya usafiri baina ya Kilindoni na Nyamisati. Kimsingi Waziri amekubaliana na hilo na naomba niwafahamishe watu wa Mafia kwamba Serikali imekubali kutuletea meli ya MV Dar es Salaam. Hivi sasa mchakato wa masuala ya kitaalam na ya kiutawala unaendelea na meli hiyo itakuwa Mafia ndani ya muda mfupi kutoka sasa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee vilevile kuipongeza Serikali, tuliomba gati na niliongea na Waziri, Mheshimiwa Mbarawa, bahati mbaya hayupo, lakini ndugu yangu Mheshimiwa Ngonyani upo nakuona hapo, tuliomba gati lifanyiwe maboresho kwa kuletewa tishari kutoka Mamlaka ya Bandari Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo furaha kuwafahamisha wananchi wa Mafia na Bunge lako Tukufu kwamba tishari lile limefika Mafia juzi, taratibu za kuli-position kwenye gati lile zinaanza na usafiri baina ya Nyamisati na Kilindoni utaboreka zaidi.
Naomba ndugu yangu Mheshimiwa Ngonyani unifikishie salamu kwa Mheshimiwa Waziri, bado tuna matatizo upande wa pili wa Nyamisati, kule maboresho bado hayajafanyika. Tunatambua kwamba Mamlaka ya Bandari ilishatenga bajeti kwa ajili ya kufanya maboresho upande wa Nyamisati. Meli hii itakayokuja kama upande wa Nyamisati hakutafanyiwa maboresho itakuwa haina maana yoyote.
Kwa hiyo, nakuomba kwa namna ya kipekee ndugu yangu Mheshimiwa Ngonyani na nikimaliza kuchangia nitakuja hapo kwako nikuelezee in details. Maboresho ya Bandari ya Nyamisati ni muhimu sana katika kuhakikisha meli ile ya MV Dar es Salaam inafanya kazi zake baina na Kilindoni na Nyamisati bila ya matatizo yoyote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa namna ya kipekee pia nikushukuru ndugu yangu, mzee wangu Mheshimiwa Profesa Muhongo. Nilikuletea concern yetu watu wa Mafia kuhusiana na kusuasua kwa mradi wa REA. Ukachukua hatua na ninayo furaha kukufahamisha kwamba nimeongea na watu wa TANESCO na tumekubaliana kwamba mradi ule utakabidhiwa baada ya mwezi Machi, hivyo basi nakushukuru sana. Pia tulinong‟ona mimi na wewe kuhusu suala la submarine cable kutoka Nyamisati kwenda Kilindoni…
Mheshimiwa Mwenyekiti, submarine ndiyo solution …
MWENYEKITI: Mheshimiwa Dau, naomba sana tuendelee kutumia lugha ya Kibunge.
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Nilikuomba Mheshimiwa Muhongo kwamba ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la umeme Mafia ni kuzamisha submarine cable kutoka Nyamisati kwenda Kilindoni.
Kimsingi ukaniambia niendelee kukukumbusha. Mimi kwa kuwa wewe ni jirani yangu hapa kila nikifika asubuhi shikamoo yangu ya kwanza ni submarine cables…
MWENYEKITI: Kwa mujibu wa Kanuni ya 60, elekeza maongezi yako kwa Mwenyekiti.
MHE. MBARAKA K. DAU: Submarine cable itakuwa ndiyo salamu yangu ya kwanza ya asubuhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema hayo, nianze sasa kuchangia Mpango. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri, Mheshimiwa Dkt. Mpango na Naibu Waziri Mheshimiwa Dkt. Ashatu wameleta Mpango mzuri sana. Mimi naamini madaktari hawa wawili watatuvusha, tuwape ushirikiano. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitajikita zaidi kwenye ugharamiaji (financing) wa Mpango huu. Mpango uliopita ulipata matatizo makubwa sana kutokana na ukosefu wa fedha. Naamini kwa ari na kasi iliyoanza nayo Serikali ya Awamu ya Tano ambapo ukusanyaji wa mapato umekuwa mkubwa sana sambamba na kubana matumizi ya Serikali, financing ya Mpango huu wa sasa haitakuwa tatizo sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, concern yangu ipo kwenye sehemu ya pili ya financing ya Mpango huu ambayo ni sekta binafsi. Sekta binafsi wanakuja kuwekeza lazima sisi wenyewe tuweke mazingira wezeshi kama mlivyosema katika Mpango wenu, kwamba ili watu waje kuwekeza hapa lazima mazingira yawe mazuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa basi, ninachotaka kusema ni kwamba tuwe waangalifu na hawa wawekezaji wanaokuja. Nitatolea mfano kule Mafia na Mzee wangu Mheshimiwa Lukuvi naomba unisikilize vizuri sana hapa, tuna Kisiwa kinaitwa Shungimbili. Mafia imezungukwa na visiwa vingi tu lakini kimoja kinaitwa Shungimbili. Kisiwa hiki cha Shungimbili kimebinafsishwa au sijui niseme kimeuzwa au sijui niseme kimekodishwa bila ya Serikali ya Wilaya kuwa na habari. Namuuliza Mkurugenzi anasema hana taarifa, namuuliza DC wangu anasema hana taarifa, naomba sana…
MWENYEKITI: Ahsante.