Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Awali ya yote, namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima. Pia nawashukuru wananchi wa Mkoa wa Rukwa kwa kuniona mimi niweze kuwawakilisha katika Bunge lako Tukufu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa umahiri wake, kwa uchapakazi wake, hatimaye kuirudishia heshima Serikali yetu. Naomba pia niwapongeze Mawaziri wote na Manaibu kwa uchapakazi wao mzuri. Hakika kweli tuna majembe na Mungu awabariki sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niunge mkono hoja nikitaka ufafanuzi wa hoja zifuatazo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Rukwa uliiunga mkono Serikali hii kwa kukipatia Chama cha Mapinduzi kura nyingi sana za kishindo. Sasa nipe nikupe!
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Mkoa wa Rukwa wanapata shida sana hasa kwenye suala la ardhi. Suala la ardhi limekuwa ni shida upande wa shamba la Efatha. Imekuwa ni kizungumkuti kwa shamba la Efatha kwa sababu mpaka sasa hivi hatujajua Serikali ina mpango gani na wananchi wanaolizunguka lile shamba. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wanapata shida sana, wamekuwa maskini, hawawezi kusomesha watoto wao kwa sababu tu ya hili shamba limechukuliwa na mtu mmoja ambaye anaitwa Efatha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imefikia wapi juu ya mgogoro huu? Huu mgogoro umekuwa wa siku nyingi sana, Wabunge wa Mkoa wa Rukwa wote wamelipigia kelele sana hili suala, lakini mpaka sasa hivi halijapata ufumbuzi wowote. Je, Serikali ina mpango gani na hili shamba? Kuna tatizo gani kulikomboa hili shamba kuwarudishia wananchi? Naiomba sana Serikali yangu sikivu ya Chama cha Mapinduzi chini ya Mheshimiwa Lukuvi, hili shamba lirudi kwa wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee pia wananchi wanaoishi uwanja wa ndege wa Sumbawanga Rukwa. Wale wananchi walifanyiwa tathmini za nyumba zao na ziliwekewa X muda mrefu, zaidi ya miaka saba. Wananchi hawa hawana urafiki tena na mabenki, wanashindwa kufanya shughuli zao za msingi kwa sababu tu hizi nyumba ziliwekewa X, wanashindwa kuzipangisha. Naomba sana Serikali iwaangalie kwa jicho la huruma hawa wananchi wa Vijiji vya Bangwe, Izia wanaozunguka uwaja ule wa ndege. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee pia hizi nyumba za National Housing. Kabla Serikali haijaanza kujenga, inatakiwa ifanye utafiti kwanza kuangalia vipato vya wananchi ili ipange bei kulingana na vipato vya wananchi. Wananchi hawawezi kuzinunua zile nyumba kwa sababu vipato vyao ni vidogo. Kwa hiyo, naomba sana Serikali iliangalie suala hili. Nawapongeza sana kwa kujenga zile nyumba, lakini zile nyumba gharama yake ni kubwa sana kiasi kwamba wananchi hawawezi kuzinunua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa haya machache, naomba Serikali iyafanyie kazi.