Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia katika Wizara hii ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka huu wa fedha 2016/2017, Wizara imeeleza kwamba inafanyia mapitio ya Sera ya Ardhi ya mwaka 1995. Mapitio haya yatakuwa hayana maana kama Wizara haitajikita kuimarisha mfumo wa utendaji wa vyombo vya usimamizi wa ardhi katika nchi hii. Hapa tunaongelea Serikali za Vijiji, pamoja na mabaraza yake ya ardhi maana yake hata kama ukiwa na sera lakini hujaviwezesha vyombo hivi ukavipa rasilimali fedha, ukavipa rasilimali watu, sera yao wanayokwenda kurekebisha itakuwa haina maana.
mamlaka hizi za usimamizi wa ardhi katika nchi yetu na kuimarisha mfumo mzima wa utendaji wa Wizara katika maeneo mbalimbali. Pamoja na marekebisho hayo ni muhimu tukaangalia masuala mazima ya wawekezaji au baadhi ya wawekezaji na viongozi na wanasiasa kuhodhi maeneo makubwa kinyume na taratibu au kuihodhi kwa kufuata utaratibu lakini wameya-damp na hawayaendelezi ni muhimu sana hili likatazamwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wawekezaji wengi baadhi yao wana-forge muhtasari wanalaghai Serikali zetu za Vijiji, wanahodhi maeneo na wanayatumia maeneo hayo kwenda kukopea benki na kudanganya au kudanganya kwamba wana mitaji lakini hawana mitaji, wanatumia ardhi hiyo kwenda kukopa benki wanafanya biashara nyingine wanatelekeza zile ardhi. Kwa hiyo, ni muhimu sana Wizara ikatazama kwa ujumla wake suala zima la hawa wawekezaji, baadhi yao wamekuwa ni wadanganyifu wakubwa wakitumia ardhi zetu vibaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kuna baadhi ya wawekezaji wanabadilisha matumizi ya ardhi kinyume na hati miliki zao zinavyoeleza, kuna wawekezaji wanapewa kwa ajili ya kilimo, anakwenda kubadilisha. Nimpe mfano Mheshimiwa Waziri, Wilaya ya Karatu, kwa taarifa ambayo tumeletewa kwenye Baraza la Madiwani kuna mashamba ambayo yanamilikiwa na wawekezaji, yametembelewa mashamba 18 ambayo yana jumla ya hekari 13,985 wengi wao mashamba haya wamepewa kwa ajili ya kilimo cha kahawa, lakini wako baadhi wamebadilisha matumizi wamejenga hoteli kubwa za kitalii, hatuna uhakika kama wamefuata taratibu za sheria za kuomba kubadili matumizi ya ardhi ile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matumizi ya ardhi ile inaonekana ni kilimo, lakini wako wengine wamejenga hoteli za kitalii maana yake ni nini? Maana yake ni pia wanaikosesha Serikali mapato, anakwenda kulipa tu kwa sababu inaonekana hati yake ni ya kilimo lakini amejenga hoteli kubwa ya kitalii analaza wageni, anapata fedha za kutosha. Kwa hiyo, ni muhimu sana Wizara ikafanya uhakiki kutembelea mashamba, ambayo jumla yako mashamba 32 ndani ya Wilaya ya Karatu yakabaini ni watu gani ambao wamekiuka taratibu za kisheria katika umiliki wao wa ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia katika hao wawekezaji wenye mashamba 32, wako wengine wameyatelekeza mashamba, wako wengine wameyaacha, wamehifadhi halafu kuna wananchi wengi pembezoni pale hawana hata maeneo ya kuzika. Mheshimiwa Waziri ningetamani aje karatu aone. Yako mashamba yanamilikiwa na Wahindi, wananyanyasa watu, wanadiriki kuwaambia hata kaya zinazokaa pale, ni marufuku kuzaana eti kwa sababu wataongeza idadi, huu ni unyanyasaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa sana Mheshimiwa Waziri afike, aone jinsi gani wananchi hawa, hawana hata maeneo ya kuzikana sasa wananchi wanakuwa watumwa katika nchi yao, haiwezekani! Hatuwezi kuthamini wawekezaji, hatuwezi kuthamini watu hao tukawapuuza wananchi wetu ambao ni damu zetu. Kwa hiyo, nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, suala hili liondoke na wananchi hawa wapate haki yao, wapate maeneo angalau hata kuweza kuzikana katika nchi yao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo nataka niongelee ni kuhusu migogoro ya ardhi. Migogoro hii ya ardhi imekuwepo kwa muda mrefu na migogoro hii mara nyingi ni kati ya wakulima na wafugaji, hifadhi na wananchi, vijiji na vijiji na kadha wa kadha kama ambavyo imeoneshwa katika hotuba yetu ya Kambi ya Upinzani. Pamoja na kwamba bado tuna migogoro lakini imepungua sana, lakini inawezekana ikaendelea kuibuka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro hii pamoja na sheria tulizonazo, lakini ni lazima Serikali ijikite katika kuimarisha vyombo vya utatuzi wa migogoro ya ardhi na lazima Serikali iangalie namna bora ya kumaliza migogoro hii ya ardhi kwa njia shirikishi na kutumia mila na desturi za maeneo mbalimbali. Hatuwezi tu kusema wakati mwingine tunafuata sheria kama ilivyo, kwa sababu mkisema mnafuata sheria kama ilivyo, ndiyo mnaua watu, mnajeruhi watu, mnafukuza watu, wakati mwingine busara itumike kwa kutumia mbinu shirikishi ya kuondoa migogoro hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano migogoro ya wakulima na wafugaji inaweza wakati mwingine kusuluhishwa kwa kutumia, mila na desturi na njia shirikishi siyo unakwenda kusuluhisha migogoro hii kwa kuchimba sijui mitaro, sijui kwa kusema wasivuke huku, haiwezekani ni lazima mtumie njia shirikishi ambayo itaweza kuondoa migogoro ya ardhi katika nchi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala moja la umiliki wa ardhi. Wapo Watanzania wengi ambao hawana hati miliki na wako wachache ambao wana hati miliki. Sababu ambazo zinapelekea hili, wakati mwingine ni urasimu na mlolongo mzima wa kupata hati hizi, kuanzia kwenye Halmashauri zetu mpaka hizo Ofisi za Kanda ambazo zinatoa hati miliki. Pia, wakati mwingine kuna rushwa kwenye halmashauri zetu, Halmashauri kule kuna shida sana kwa hao Maafisa Ardhi. Hizi rushwa zinawanyima wananchi haki ya kupata ardhi yao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niishauri Serikali muandae programu maalum ya kuhakikisha mnakopesha wananchi, yaani kuliko mwananchi atafute fedha ya kuingia gharama ya hatua hizi mpaka apate hati, mnaonaje mkiwa na programu maalum, Serikali ikagharamia, mkawakopesha wananchi wakawa na hati zao, wakalipa kidogo kidogo mpaka akamilishe deni lile, ili tuhakikishe wananchi walio wengi wanapata hati, maana yake hati hizi wakipata mwisho wa siku wanalipa mapato, inakuwa ni sehemu ya mapato ya Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie jambo la mwisho, kuhusu ulipaji wa fidia pale ardhi inapotwaliwa. Jambo hili mmeeleza kwamba mmeanzisha Mfuko huu wa kutoa fidia ambayo itaanzia na bilioni tano. Ni muhimu sana Serikali ikawalipa wananchi fidia kwa wakati, ikawashirikisha wananchi katika…
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.