Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kupata fursa hii, nimshukuru Mwenyezi Mungu na familia yangu na chama changu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme suala la ardhi kwa Dar es Salaam halijaonekana kupewa kipaumbele kama inavyostahili. Ndugu zangu sote tunajua Dar es Salaam ndiyo Tanzania, wote tunajua changamoto zinazoikuta Dar es Salaam zinasambaa katika mikoa mingine. Dar es Salaam ikiwa mbovu, Dar es Salaam ikiwa ndiyo chanzo cha migogoro, Dar es Salaam ikiwa haitamaniki, tunategemea kwamba sura ya Tanzania itapotea. Ndugu zangu tunavyoongea leo Dar es Salaam ambayo ina population zaidi ya watu milioni nne inatumia master plan ya mwaka 1977. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeendelea kukosa master plan mpya tukitumia master plan ya population iliyokuwepo wakati ule, leo miaka mingi inayofuatia tunatumia plan zile zile. Maeneo yameendelea kuwa machache, watu wamevamia maeneo yote yale yaliyokuwa wazi, maeneo ya mabondeni, maeneo yamekwisha Dar es Saalam imegeuka jiji ambalo siwezi kujua hata nilisemaje. Naona changamoto kubwa zinazotokea hapa ni kutokana na kushindwa kwa Wizara ya Ardhi kusimamia kikamilifu kitovu cha ardhi ambacho ni Dar es Salaam.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina kilio kikubwa cha wananchi wa Msimbazi, mimi ninatokea katika Mkoa wa Ilala, naongelea Ukonga, naongelea Ilala, naongelea Segerea. Tunapita pale mto Msimbazi, mto ule una ukubwa wa hekari takriban 1,900 ume-cover eneo kubwa la makazi na katika Jimbo la Segerea ni Kata sita ambako kuna wakazi takriban 3,000. Mheshimiwa Waziri haya ni majina ya wakazi ambao majina yao yaliwekewa X, hawa wananchi wameishi mabondeni kuanzia miaka ya 1970, wameishi katika bonde la Mto Msimbazi likiwa bado ni bonde dogo. Nasema mto Msimbazi una ukubwa kuanzia Pugu kuja mpaka daraja la Salander, ni eneo kubwa sana takriban ekari 1900 kwa hiyo ni wakaazi wengi sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati ule walikuwa wananchi wachache na bonde lilikuwa dogo kwa sababu baada ya muda bonde limeendelea kupanuka, kwa hiyo wakazi wameendelea kuwa wengi, lakini bonde limeendelea kula sehemu kubwa ya makazi ya watu.
Mheshimiwa Mwenyekiti mwaka 1972 Serikali ikaridhia kwamba watu wanaoishi katika mabonde au kwenye squatter areas watambulike kama makazi halali na wananchi wangu katika Jimbo la Segerea na maeneo mbalimbali wakatambuliwa ndiyo maana wengine wakaja kuwa na leseni za makazi. Mheshimiwa Waziri mwaka 1979 eneo lile linakuja kuwa declared kwamba ni hazardous area bila kuangalia kwamba kuna watu walikuwa wanaishi pale ambao wanapaswa kuhamishwa kupelekwa sehemu nyingine. Hiyo compensation na kuwaondoa haikufanyika, wananchi wakaendelea kuishi katika eneo hilo. Kuanzia mwaka 1972 imehalalishwa, mwaka 1979 mnasema ni hazardous area bila kusema watu mnawa-locate wapi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi tukasikia Waziri wa Mazingira Mheshimiwa January Makamba kupitia NEMC wakaenda wanabomoa, wakaenda wanaweka X katika maeneo ya watu ambao wamekuwa wanaishi pale hawajapewa fidia, bonde limepanuka, ilikuwa ni mita 60 leo watu karibu wote wanajikuta kando kando mwa mto kwa sababu mto umepanuka bila kuwapa fidia. Hawa wananchi, Waziri wanaoteseka na kufukuzwa na kuwekewa X wasijue pa kwenda, ni watu ambao wanalipa kodi kwenye Wizara hii, ni watu ambao Wizara inawatambua kama wakazi halali kwa maana wana leseni za makazi. Sasa tunaomba tujue huo mkanganyiko umekaaje? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mnadhani ile ni hazardous area na wale ni wananchi halali kwamba wamepewa leseni za makazi tunaomba wapewe fidia. Nimeendesha kesi pamoja na wananchi wangu bahati mbaya kesi yetu imetolewa mahakamani kwa kukosa procedure lakini tunaamini Wizara kupitia kwa Mheshimiwa Waziri haki ya wananchi wanaoishi katika Mto Msimbazi inapaswa kupatikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti,Kama tunadhani yale makazi sio halali na sisi pia tunakiri kwamba siyo makazi halali wapewe maeneo mbadala wakajistiri. Kupata ardhi Dar es Salaam ni kazi kubwa sana wote mnajua. Ardhi imepanda thamani lakini pia wanaoishi kule ni watu ambao wana maisha duni. Tunavyowaondoa tunataka waende wapi kama hatuwapi makazi mbadala? Hilo ni la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kuna wakazi wa Kipunguni, Kipunguni B na Kipunguni Mashariki, nimefurahi kwamba huo mgogoro umeshafika kwa Waziri na natamani huo mgogoro ufanyiwe kazi kwa sababu umedumu muda mrefu. Huo ni mgogoro kati ya wananchi hawa tangu mwaka 1997 wakipambana na mamlaka ya Airport ambayo ilifanya tathmini ya kiujanja ujanja , ikiwakumbatia watu wachache na kuwapa vihela ambavyo tunaviona kama hongo na kuwahamishia maeneo ya Buyuni ambako walipelekwa na kule hawakupewa viwanja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hapa tuna wananchi wa Kipunguni A na Kipunguni Mashariki ambao wanaishi katika eneo ambalo unaambiwa ni Mamlaka za Airport hawaruhusiwi kuendeleza hayo maeneo, lakini wale wachache ambao wamekuwa reallocated wamepelekwa Buyuni bila kupewa maeneo ina maana wamekuwa dumped pale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu mwaka 1997, 1998 watu wanaishi kwenye mahema katika maeneo yale. Wanawake wanateseka, watoto wanateseka na Serikali ipo. Mamlaka nyingi zimejaribu kuingilia akiwepo Mkuu wa Wilaya ya Ilala, ikiwepo mimi Mbunge, wakiwepo Madiwani mbalimbali lakini huo mgogoro umeshindikana na wale wananchi ni wanajeshi wastaafu waliotumikia nchi, lakini bado wameendelea kupigwa danadana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kesi yangu ya tatu naongelea viwanja vya wazi, Dar es salaam viwanja vyote vya wazi vimevamiwa. Waziri Lukuvi amegawa ramani za ardhi katika mitaa mbalimbali ya Dar es Salaam, asilimia 80 maeneo ya wazi yamevamiwa na maofisi ya CCM, yamefanywa kuwa pupping place, kama Mheshimiwa Waziri ametoa ramani anatusaidiaje ili hayo maeneo ambayo yamekuwa allocated ni ya wazi yarudishwe kwa umma? Tunataka kufanya maendeleo sisi, tunataka watoto wakapate viwanja vya kuchezea, tunataka kujenga vijana wakafanye ujasiriamali kwenye maeneo husika. Tunaomba maeneo yarudishwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo mengine ya wazi mfano mdogo ni kutolewa kwa eneo la Coco Beach, Mheshimiwa Waziri tunaomba atueleze eneo la Coco Beach limeuzwaje? Wakati Dar es Salaam nzima watu wote tunakwenda kupumzika Coco Beach leo anapewa mwekezaji katika misingi ipi wakati Mheshimiwa Waziri akiwa Waziri. Tutaomba tupewe majibu ya msingi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kitu cha tatu au cha nne ambacho ni kero kubwa ni utozaji wa gharama inaitwa gharama ya premium katika ku-process hati za ardhi. Hiyo gharama imekuwa ni kubwa ambayo ni seven point five katika kila anaye-process umilikaji wa ardhi anapaswa kulipia. Hiyo gharama inaendelea kuwa kubwa na kuzidi ku-discourage watu kupima maeneo au kurasimisha maeneo na wakishindwa kurasimisha maeneo maana yake Serikali itakosa mapato. Kwa hiyo, ni lazima tuangalie ni akina nani wanakusanya hiyo pesa? Hiyo pesa inakwenda wapi? Naomba Waziri aje na majibu hayo ya kuridhisha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ni mgogoro wa msitu wa Kazimzumbwi ambao uko katika Jimbo la Ukonga. Huo mgogoro upo tangu mwaka 1994. Watu wakigombania mipaka, wananchi wanagombania mipaka dhidi ya hifadhi ya maliasili, maliasili wanakataa kutambua mipaka ambayo imewekwa na Manispaa pamoja na Wizara kuwa imetambua lakini Maliasili wanakuja leo wanasema hatuwatambui. Uhusiano wa wananchi pamoja na hiyo hifadhi imekuwa ni wa shida sana, wanaotoka kwenda upande wa pili wanawake wanabakwa watu wanapigwa mapanga imekuwa ni changamoto…
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.