Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Jehova kwa kunifanya hivi nilivyo, nayaweza yote katika yeye anitiaye nguvu.)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu leo ni mara yangu ya kwanza kuchangia, nachukua fursa hii kuwashukuru sana wapiga kura wangu wote wanawake wa Mkoa wa Mbeya wa Chama cha Mapinduzi kwa kunichagua kwa kura nyingi sana za kishindo, na mimi nasema sijawaangusha na ninawaahidi sitawaangusha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia nimshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sera yake nzuri sana ya Hapa Kazi Tu na hakika sasa ni kazi tu. Naomba nichukue fursa hii nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Ardhi na dada yangu Mheshimiwa Angeline pale. Nakumbuka kazi ni nzuri, tulikuwa tunamwombea Mheshimiwa Waziri aifanye kazi hii arudi tena kwenye cabinet na katika Wizara ile ile kutokana na jinsi alivyokuwa ameinyoosha vizuri Wizara hii. Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni. Mheshimiwa Waziri, hongera lakini gema likisifiwa sana, tembo hulitia maji. Kaza buti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya utangulizi huo, naomba niseme tu kwamba Mheshimiwa Waziri tunakupongeza, umetuletea haya makabrasha na timu yako nzima, lakini naomba in future usituletee siku ile ile unayo-present bajeti yako kwa sababu tunahitaji muda tuweze kusoma, kuperuzi na kuishauri Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mwalimu Nyerere katika concept yake ya uchumi alisema ili tuendelee tunahitaji mambo manne; tunahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Mojawapo ya sifa ya Tanzania tunayojivunia ni ardhi. Ardhi yetu ni kubwa na ni nzuri sana lakini cha kushangaza na cha ajabu ni migogoro isiyokwisha, ni migogoro ambayo kwa kweli ni so much rampant. Nikuchukulia mfano wa kule kwetu Mbeya, kipaumbele chetu sisi Wanambeya ni ardhi; asubuhi, mchana, jioni. Ukiangalia, hii ardhi iko kwenye kilimo, viwanda, elimu, biashara, kila kitu, vyote vinahitaji ardhi. (Makofi)
Mheshimiwa Waziri, kaka yangu Mnyalu ulikuja Mbeya na umejionea mwenyewe, migogoro ya ardhi iko vibaya sana hususan ule uwanja wa ndege wa zamani. Hata katika maeneo yale yenye makazi holela, ukichukulia pale Iyunga, Mwakibete, Ilemi, Nzovwe, kote na maeneo ya Isanga mbalimbali, ni migogoro mitupu. Nilikuwa naomba ukisimama hapa unapo-wind up utupatie status mpaka sasa hivi maelezo yake ya kina, Serikali katika kuboresha mpango huu ambao ni tatizo sugu kwa Wanambeya imefikia wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ni-declare mimi nilikuwa Mwenyekiti wa hii Kamati, naomba nizungumzie suala zima la Intergrated Land Management Information System. Mheshimiwa Waziri alitupeleka Uganda katika kusomea na kujifunza jambo hili. Wenzetu Uganda wako mbali sana katika suala zima la electronic, hati unaitoa within a day, unaipata siku hiyo hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nawashukuru ndugu zetu wa World Bank wameweza kusaidia project hii ambayo mpaka sasa hivi nilikuwa nataka Mheshimiwa Waziri katika ukurasa wake wa 27 ambapo amezungumzia hili jambo, lakini hajatueleza ni kwa nini hili jambo limechelewa sana mpaka leo hii na lini lita-kick off? Tunataka maelezo ya kina, maana yake tumeambiwa tu project, project; World Bank, World Bank! Mpaka sasa hivi hatujajua nini hatima yake. Tunahitaji maelezo ya kina atakapokuja hapa ku-wind up.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie suala la maeneo ya wazi, maeneo ya Mashamba pori makubwa ambayo yametelekezwa kwa muda mrefu. Nilikuwa nataka kujua nini mkakati wa Serikali katika masuala haya ukizingatia kwamba hata Land Bank hatuna. Land auditing hatujui inafanyikaje! Tunahitaji tunapoelezwa sisi kama Wabunge, tuelezwe maelezo ya kina ambayo sisi hatutakuwa na maswali mengi. Tusiwe tunapigwa blah blah za kisiasa tu hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo yote, naomba nizungumzie suala zima la mradi ule wa Kigamboni. Huu mradi naomba niseme ni non-start up kwa sababu hii project ambayo tunaizungumzia, pesa inapotea bure tu. Huu mradi ni bora ukavunjwa kabisa, ukarudishwa kwa wananchi wa Kigamboni na Manispaa ya Kigamboni kwa sababu hauna faida. Wizara kwanza ni kubwa sana, resources nyingi zinapotea. Hii Wizara iwe ni eyes on, eyes off; hatuhitaji kwamba iendelee kushikilia mradi wa Kigamboni ambao tayari umeshafeli. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri atakaposimama hapa atueleze mkakati mzima, hii KDC haina haja, wala Wizara isihangaike nayo, huu mradi uvunjwe kabisa urudishwe kwa wananchi kule Kigamboni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni sambamba pamoja na Tume ya Matumizi Bora ya Ardhi...
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba utunze muda wangu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni sambamba na Tume ya Matumizi Bora ya Ardhi, nimeona wamepewa vote sawa sawa, lakini tukumbuke nini sababu ya kuunda Tume? Tume inapoundwa, lazima kuwe na mpango maalum wa kazi maalum, lakini Tume hii mpaka sasa hivi hatuoni hata umuhimu wa hii wake. Lazima tuseme, ikiwezekana irudi Wizarani ipewe directorate iwe ni kama Idara. Tunahitaji effectiveness ya Tume hii na lazima tunapozungumzia Hapa Kazi Tu, basi tuzungumzie na masuala ya results oriented. Siyo tu kwamba kuna Tume, halafu resources zinapotea bure; na ukizingatia Tume hii imedumu kwa muda mrefu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nahitaji pia Mheshimiwa Waziri atueleze hili suala la zima la D by D ambalo ni muhimu sana, litakuwaje katika Wizara hii ya Ardhi, ukizingatia kwamba D by D na umuhimu wake ukishafikiwa, basi ni utaratibu tu maalum unaotakiwa kufanyika kwa sababu naelewa kuna pros na cons zake katika hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu suala la Shirika la Nyumba. Shirika la Nyumba tunaelewa ni kweli wana management team ambayo ni very much creative na wame-reform kwa sana na shirika lina surplus, lakini Waheshimiwa Wabunge wote hapa ni mashahidi, Watanzania wote ni mashahidi; Shirika hili la Nyumba wakilala, wakiamka wao ni nyumba. Maisha yao siku zote ni nyumba na Watanzania wanaelewa hivyo. Tatizo kubwa, bei yao ya nyumba ni kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi leo humu ndani tujiulize, ni Watanzania wangapi na wa kawaida ambao ndio asilimia kubwa, wamefaidika na bei ya Shirika la Nyumba? Nasema, viongozi hawa wa Shirika la Nyumba ambao wengi wanatoka kwenye corporate world, wabuni zaidi jinsi ya kupunguza bei...
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Mwanjelwa.