Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa afya na kunipa uwezo wa kuchangia leo. Naomba nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuwa na imani kubwa kwa kumteua Mheshimiwa Profesa Muhongo kuwa Waziri na Mheshimiwa Dkt. Matogolo kuwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, uamuzi wa kupeleka asilimia 40 kwenye maendeleo kwa Wizara ya Nishati na Madini; napongeza kwa juhudi kubwa katika sekta zote za nishati na madini. Naomba nianze na suala la nishati; kwanza nishukuru kwa mradi wa REA, katika Wilaya ya Babati maeneo yanayotarajiwa kupata nishati hii tayari wananchi wameanza kujipanga kutumia kwa maendeleo. Katika REA II maeneo mengi yameachwa, tunaomba na nashauri, katika Mpango wa REA III hayo maeneo na taasisi muhimu yapatiwe umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri Wizara kupitia TANESCO itusaidie kupitisha design ya nguzo za cement za umeme ili tuweze kuanza kuzalisha. REA III itahitaji nguzo nyingi sana, tukiruhusiwa sasa uzalishaji baada ya design kukubalika itatusaidia kufanya matayarisho mapema.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba Wizara isaidie kufuta (charges) gharama ya kutotumia umeme katika mradi wa kilimo na viwanda vya kuongeza thamani ya mazao yetu ambayo viwanda hivyo hufanya kazi kwa miezi miwili au mmoja tu pamoja na umwagiliaji. Tozo hiyo inaua viwanda na sekta ya kilimo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri Serikali iangalie namna ya kuongeza tozo kwenye mafuta, napendekeza iongezwe sh. 200/= kutokana na bei ya mafuta ya dunia imeshuka sana. Hakuna nauli, usafiri au bidhaa iliyoshuka, hawana kodi iliyoongelea kutoka kwa wafanyabiashara, ikiongezwa sh. 200/= kwa lita, sh. 70/= iende REA, Umeme Vijijini, sh. 70/=; Maji Vijijini, sh. 40/= iende Mfuko wa Utafiti na sh. 10/= Mazingira. Bei ya mafuta ikipanda duniani, basi tozo hii ipungue kidogo kidogo. Tunaweza kupata takribani shilingi bilioni 330 kwa miezi sita. Kwa hiyo, wastani wa shilingi bilioni 110 kwa Nishati Vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia, nashauri Serikali iondoe Kodi ya VAT kwenye vito na vidani (germstone and jewelry) vinavyouzwa ndani ya nchi (local sale). Kama bei ya dunia ya dhahabu inajulikana na vito kuweka VAT inafanya sekta isikue. Nashauri kituo cha Arusha cha Mafunzo kiboreshwe na mafunzo ya kuchonga vito na kutengeneza vidani (jewelry and lapidary) ianze mapema. Napongeza juhudi za Wizara kwa sasa. Ahsante.