Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri binafsi, Naibu Waziri na Watendaji wote kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba katika REA III vijiji 23 vifuatavyo vipatiwe umeme, ili waweze kwenda na kasi ya maendeleo sawa na maeneo mengine:-
Vijiji vya Lutongo, Kabusungu, Kilabela, Kilino, Isanzu, Igogwe, Shibula, Bulyanhulu, Ilalila, Chabakirua, Masemele, Igombe A, Igombe B, Mhonze A, Buganda, Zenze A, Zenze B, Iseni, Ilekako, Igalagale, Kasamwa, Imalang‟ombe na Isesa. Kazi mnayoifanya ni nzuri sana na inatia moyo, endeleeni kuchapa kazi msikatishwe tamaa na watu wasioitakia mema nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeambatanisha Shule za Sekondari zisizo na umeme. Naomba zipatiwe umeme maana ziko nje au vijijini; Mwinuko, Nundu, Kilimani, Shibula, Kirumba, Kabuhoro, Kangaye, Ibinza, Lukobe, Mihama na Sangabuye.