Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Mufindi Kusini tunaomba umeme katika Kata za Mtambula, Maduma, Idunda, Kiyowela, Magunguli, Itandula, Idete na Mninga. Pia, naomba umeme upelekwe kwenye Vituo vya Afya Kihanga, Mninga, Mtwango na Udumuka.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kwenye taasisi ni muhimu sana kupata umeme naomba sana shule za msingi, sekondari na taasisi za kidini kupelekewa umeme. Jimbo la Mufindi Kusini tuna tatizo kubwa la umeme, tunaomba Serikali ipeleke umeme katika Jimbo la Mufindi Kusini; vijiji vingine nyaya zimepita juu kwenye nyumba za watu, tunaomba Serikali kuangalia kwa huruma vijiji hivi, kwa mfano Kijiji cha Rugolofu, Kitasengwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, naipongeza Serikali kwa kufuta Service Charge na kupunguza gharama za uingizaji wa umeme katika nyumba.