Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, umeme kukatiza maeneo machache tu ya mjini (REA) huku vijiji vingi vikibaki bila umeme.
Mheshimiwa Spika, nguzo za REA/umeme zimewekwawekwa tu bila kufuata barabara na mara nyingi zinakatiza katika viwanja vya watu.
Mheshimiwa Naibu Spika, fluctuation ya umeme kitu kinachoshusha rate/quality za uzalishaji viwandani.
Mheshimiwa Naibu Spika, nguvu ndogo na bajeti ndogo kuwekwa katika joto ardhi, nishati inayoonekana ni ya gharama nafuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa mapendekezo kwa Serikali juu ya hitaji la msingi la kutumia transformer za TANELEC kwa lengo la kupunguza gharama ambazo Serikali inaingia kwa kununua transformer za China/India wakati Tanzania ina hisa kwenye hiyo kampuni.
Mheshimiwa Naibu Spika, pesa nyingi imetoka kwa mwaka 2015/2016, lakini bado changamoto za umeme ziko dhahiri. Hivyo, ama usimamizi ni mbovu au miundombinu hii haiwagusi watu moja kwa moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, napendekuza kushushwa nishati ya gesi kwa lengo la kuleta unafuu wa maisha kwa wananchi wanaoitumia.