Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, umeme ni kitu muhimu sana kwa maendeleo ya nchi yetu na ajira kwa wananchi wetu. Bado naendelea kuzungumza kuhusu Mikoa ya Pembezoni kwa kuchelewa kupata umeme wa uhakika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Rukwa tunao umeme wa jenereta unaosaidiana na umeme kutoka Zambia ambao una changamoto zake, naomba Serikali kuona umuhimu wa kutuunganisha na grid ya Taifa kutokea Mbeya.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la usambazaji wa umeme vijijini huu wa REA, tukaongeze kasi kwa mikakati maalum kuharakisha vijiji vya mipakani kupata umeme huo, Kata zifuatazo Kabwe, Mirando, Kipili, Wampembe, Kala, Kasanga, Wampambwe, Sopa, Katete, Mambwenkoswe. Vilevile vijiji vya Bonde la Rukwa ukizingatia ni wakulima wazuri wa mpunga na alizeti wanahitaji kuwa na mashine za kukoboa mchele na kusindika alizeti.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni wazi kuwa bajeti ya nishati haikidhi mahitaji kwa Mkoa wa Rukwa, baada ya kukamilika kwa barabara ya Tunduma, Sumbawanga ambayo ni mwanzo wa kufunguka Mkoa wa Rukwa. Naomba Serikali kuangalia Mkoa huu kwani unahitaji kupiga hatua kwa maendeleo ya wananchi wake.