Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru Mungu kwa kunipa afya ya kuweza kuchangia hotuba hii ya Wizara ya Nishati na Madini
Mheshimiwa Naibu Spika, nishati ya umeme ni nusu ya maisha ya binadamu hasa kwa wanawake kwa sababu mwanamke ni mdau mkubwa ndani ya nyumba; ikiwa umeme hamna au gesi basi kwake ni mtihani, itabidi afunge safari kutafuta kuni ili familia waweze kupata chakula.
Mheshimiwa Naibu Spika, mazingira ya ukataji wa miti kwa ajili ya kuchoma mkaa ili aweze kupikia au kufanya biashara. Miti inakwisha na nchi inakuwa na ukame kwa sababu ukataji wa miti unaharibu vyanzo vya maji na wafugaji wanahangaika kutafuta maji kwa ajili ya kuharibika kwa mazingira.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu madini, wachimbaji wadogo wadogo: Watanzania wengi ni wachimbaji wadogo wadogo ndiyo ambao wana mchango mkubwa katika kulipatia Taifa mapato.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali hutoa ruzuku kwa wachimbaji wadogo ili waweze kujiimarisha katika kazi zao, lakini la kusikitisha ruzuku hizi haziwafikii walengwa na kuanza kutoa malalamiko, mfano maeneo ya Mwanza, Geita na kadhalika. Naishauri Serikali iunde Kamati ya kusimamia jambo hili, ikibainika wahusika washughulikiwe, hayo ndiyo majipu ya kushughulikiwa kutumbuliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nishati ya mafuta ni muhimu sana katika maisha ya binadamu kama ilivyokuwa maji ni muhimu katika maisha ya binadamu na mafuta ni hali kadhalika, kwa sababu mafuta tunaendeshea magari, meli, ndege na pia kuendesha mitambo, kama hakuna umeme yanatumika kwenye jenereta. Hivyo, nishati ya mafuta inaleta uchumi katika Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kusikitisha nchi hii haina formula ya bei maalum. Ukienda Dar es Salaam bei nyingine, Unguja bei nyingine, Ukienda Mtwara bei ni nyingine na nchi nzima bei hazilingani.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaiomba Serikali ipange mpango maalum kwa kupanga bei ambayo inalingana ili wafanyabiashara wasiwanyonye wananchi, wengine ni wanyonge katika nchi hii wanahitaji kuangaliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kutoa mchango huu, naomba kuwasilisha.