Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Rashid Mohamed Chuachua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. RASHIDI M. CHUACHUA: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi kubwa na nzuri ya kusambaza na kusimamia nishati ya umeme. Hata hivyo, naomba ufafanuzi Mheshimiwa Waziri atakapofanya majumuisho katika maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kuwa chanzo cha nishati ya umeme wa gesi katika Mkoa wa Mtwara, hali ya usambazaji wa umeme hairidhishi. Pale ambapo umeme umefika hali ya kukatikakatika kwa umeme inaendelea kuwakatisha tamaa wananchi wa Mikoa ya Kusini hususani Wilaya ya Masasi. Kwa kweli ikiwa nishati ya mwanga wa kibatari inayoweza kuzimika kwa upepo wakati wowote inapaswa iwe tofauti na ile ya umeme. Kwa sisi watu wa Masasi inatuwia vigumu kutofautisha kutokana na kukatikakatika kila wakati bila ya taarifa yoyote.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri atueleze hali hii itakwisha lini? Je, Serikali haioni sababu ya kuwa na njia mbadala ya umeme ambayo kwa sasa umeme unaokuja Masasi unapitia Tandahimba, Newala - Masasi kuelekea Nanyumbu? Matatizo yoyote ya umeme katika maeneo hayo yanatuathiri mara kwa mara wananchi wa Masasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunalo tatizo kubwa la kutofanyiwa marekebisho au matengenezo ya nyumba za wafanyakazi wa TANESCO zilizopo katika Kata ya Migongo, Jimbo la Masasi. Nyumba hizi zinageuka kuwa magofu wakati watumishi wanahangaika mahali pa kukaa. Naomba nijue mkakati wa Serikali kuhusu nyumba hizi ?
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.