Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Profesa Muhongo pamoja na Naibu Waziri kwa hotuba na kazi nzuri wanayoendelea kufanya. Kwa bahati mbaya sitapata nafasi ya kuchangia, yangu ni machache.
Mheshimiwa Naibu Spika, Karagwe Vijijini ina vijiji 110 na kila kimoja bado kinahitaji huduma ya REA III. Orodha ya vijiji tayari tumeshawasilisha Wizarani, naomba sana Karagwe ipate REA III kuanzia Julai, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, Upinzani wamekuwa objective na ushauri wao naomba tuuzingatie hasa:-
(a) Mapitio ya mikataba ya umeme wa emergency;
(b) Energy Mix Policy or National Energy Policy isisahau hydro-power bado ni potential na environmentally friendly tuipe weighting ya kutosha;
(c) Hoja za wachimbaji wadogo zina mashiko;
(d) Dira ya STAMICO tuiangalie na tuizingatie whether kupewa tail- end production segment ni economical kwa STAMICO;
(e) Mfuko wa abandonment cost and environmental rehabilitation haupo wazi, ni vema Serikali ikatoa maelezo ya uendeshaji wake; na
(f) Sheria ya Watumishi iweke katazo kwa Watumishi wanapostaafu kujiunga na kampuni za nishati na madini kwani kwa hali ilivyo sasa ina-attract rent seeking behavior.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.