Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuipongeza Wizara hii kwa hotuba nzuri iliyojieleza vizuri kwa maslahi ya Watanzania kwa ujumla, pamoja na yote naomba Serikali iweke makazi katika suala lifuatalo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana hasa katika maeneo yanayozunguka migodi yetu. Suala hili limesababisha mauaji ya vijana hawa wanaparamia migodi kuweza kupata chochote kama tunavyosikia mara kwa mara kwenye mgodi wa Nyamongo, Mkoani Mara.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niishauri Serikali yangu sikivu, Serikali inayotekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi inayoahidi kupanua wigo wa ajira kwa vijana, iweke mikakati maalum ya kuhakikisha kwamba, migodi mikubwa kama Nyamongo inauza mchanga ambao hauhitajiki na mgodi kwa wananchi ili nao waende kusafisha na kupata japo kidogo katika rasilimali yao.
Mheshimiwa Naibu Spika, naamini suala hili linawezekana na naamini kwamba, Serikali hii, haitashindwa kuweka utaratibu huu wa wananchi kupata mchanga huo kutoka migodini.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja.