Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri, kwanza kabisa nakupongeza kwa hotuba yako nzuri. Pili, naunga mkono kwa asilimia mia moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kuunga mkono hoja hii naomba nichangie maeneo yafuatayo:-
(i) Sekta ya Umeme, suala la kukatikakatika kwa huduma ya umeme Wilaya za Mpwapwa, Kongwa, Gairo; je, ni sababu gani zinazofanya umeme kukatikakatika katika Wilaya hizo na kusababisha vitu vingi kuungua. Mheshimiwa Waziri ana maelezo gani kwa wananchi wa maeneo hayo kwa kuwa ni kero kubwa sana.
(ii) Je, Serikali ina mpango gani wa kuvipatia umeme Vijiji vya Makutupa, Bumila, Mbori, Inzomvu, Tambi, Mlembule, Mwenzele, Nana, Mafuto, Majani, Mugoma, Mzogole, Kisisi, Sazima, Igoji Kusini (Isalaza), Chamanda, Kiboriani, Makanana, Chibwengele, Pandambili (Jimbo la Mpwapwa) Makawila, Chimaligo, Kazania, Kiegea na Ngalamilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sekta ya Madini, kwa kuwa Wilaya ya Mpwapwa kuna Wachimbaji wadogo wadogo Vijiji vya Winza (wanachimba rubi), Tambi, Mlembule (wanachimba copper) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wachimbaji wadogo wadogo wa Wilaya ya Mpwawa ili waboreshe hali ya uchimbaji wa madini kuliko hivi sasa wanatumia vifaa duni. Je, Mheshimiwa Waziri au Naibu watatembelea lini Wilaya ya Mpwapwa ili kukutana na wachimbaji wadogo wadogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja hoja hii na kumtakia Mheshimiwa Waziri kila la heri, bajeti yake ipitishwe na Bunge hili Tukufu.