Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, naanza kwa kuunga mkono hotuba ya Waziri. Pia naipongeza Serikali kwa mipango yake mizuri ya kusambaza umeme nchi nzima hata huko vijijini ili kuchochea maendeleo kwa wananchi na kuongeza pato la Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Nyang‟hware lina kata 15 na vijiji 62 hadi leo hii ni kata mbili zimefikiwa na umeme, nazo ni Kata ya Khalumwa na Nyang‟hware. Hata hivyo, Kata ya Khalumwa ndipo yalipo Makao Makuu, ni Kijiji kimoja tu ndiyo kina umeme. Pia Kata ya Nyang‟hware ni kijiji kimoja tu ndiyo umeme umefika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Busolwa tayari line imeshafika, lakini umeme haujawaka. Pia Kata ya Nyijunau nyaya za umeme zimepita juu kuelekea Kata ya Nyang‟hware ila Nyijundu haina umeme. Kata ambazo hazina kabisa umeme ni hizi: -
Kata ya Bukwimba na vijiji vyake; Kata ya Nundu na vijiji vyake; Kata ya Izunya na vijiji vyake; Kata ya Kafita na vijiji vyake; Kata ya Kakora na vijiji vyake; Kata ya Nyijundu na vijiji vyake; Kata ya Busolwa na vijiji vyake; Kata ya Kaboha na vijiji vyake; Kata ya Shabaka na vijiji vyake; Kata ya Mwingiro na vijiji vyake; Kata ya Nyaburanda na vijiji vyake; na Kata ya Nyamtukuza na vijiji vyake.
Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali, tukiipitisha bajeti hii umeme upelekwe kwenye kata hizo, nitashukuru sana.