Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Risala Said Kabongo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia Wizara ya Nishati na Madini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na tatizo kubwa la ukataji wa miti na kuvamia mapori kwa ajili ya uchomaji wa mkaa baada ya ujangili wa wanyama sasa ni ujangili wa misitu. Namtaka Waziri atoe majibu ni namna gani Serikali hii kupitia Wizara hii imejipanga kuzuia au kupunguza matumizi ya mkaa hasa mijini ambako kuna nishati mbadala ya gesi na soko kubwa la mkaa limeelekezwa huko.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukataji wa miti kwenye mapori umeendelea kusababisha mabadiliko ya tabianchi ambayo yanasababisha mafuriko sehemu kubwa nchini. Mafuriko haya yanatokana na ukataji wa miti ambayo huzuia kingo za mito na hivyo kusababisha mafuriko makubwa. Namtaka Waziri atoe majibu ya kina ni namna gani amejipanga kuokoa misitu kwa kwa faida ya kizazi cha sasa na kizazi kijacho.
Mheshimiwa Naibu Spika, namtaka Waziri atoe majibu ni kwa namna gani Serikali imeweka mkakati wa kudhibiti wachakachuaji wa mafuta ya magari ili kuondokana na adha ya uharibifu wa magari.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunashuhudia matumizi ya solar kama umeme mbadala maeneo mengi nchini na hasa mijini. Namtaka Waziri anipe majibu ni kwa namna gani zinaweza kusaidia wananchi wa vijijini ili watumie nishati hii kwa wingi kwa kuuza solar kwa bei nafuu kwenye maduka ya Serikali ili wananchi wengi wafaidike na nishati hii. Naomba Waziri anipatie majibu haya kwa faida ya wananchi wetu wa vijijini.