Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Livingstone Joseph Lusinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtera

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mungu kwa kupata muda, lakini mimi siyo wa kuzungumza dakika chache ila nitajitahidi maana mara nyingi huwa napiga hapa nusu saa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Dkt. Mpango kwa kuleta taarifa nzuri. Nianze na suala la viwanda mimi nizungumzie kilimo cha biashara. Ni vema Serikali ikajikita kwenye kuanzisha viwanda vidogo ili wakulima hasa wa matunda, badala ya makampuni yanayotuuzia juice kununua juice nje ya nchi, yanunue matunda yetu ya ndani. Tukifanya hivyo tutakuza na tutakuwa na kilimo cha biashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niseme watu wamekuwa wakizungumza sana humu ndani ya Bunge, wanazungumza kuhusu Polisi kuingia humu ndani. Nataka leo nisimame kuwatetea Polisi kwa sababu wao hawawezi kuja humu. Polisi ukimwona mahali popote kaenda kama Field Force, ujue ameitwa na watu wa eneo hilo. Wabunge, tuache tabia ya kuwaita Polisi, ukifanya fujo unawaita Polisi, na Polisi wameshaingia Kanisani wakati wa mgogoro ule wa Dayosisi ya Pare, Polisi wameshaingia Msikitini wakati wa fujo, Polisi wameshaingia Bungeni baada ya Wabunge wa Upinzani kuanzisha fujo. (Makofi)
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ukimwona Polisi kaingia mahali ujue kaitwa, na kama ninyi ni wageni hamuelewi utaratibu wa humu ukianzisha fujo umeita Polisi. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua kuna watu wamekuja hapa bado hawajapigwa semina, kwa hiyo ngoja leo niwaelimishe. Mmesema vizuri na mfano uliotolewa na Mheshimiwa Heche hapa mdogo wangu ambaye mimi nimemfundisha siasa, kwamba eti anataka kulinganisha Chama hiki na kina Hitler, lakini leo nawaambia Chama chochote cha Upinzani duniani kikishindwa kushinda uchaguzi katika vipindi vitatu, kinageuka kuwa chama cha kigaidi, ndiko wanakoelekea hawa. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa ndipo wanapoekelea, maana kinakuwa chama sugu, kinakuwa Chama cha Upinzani sugu, tulikubaliana wakati ule, kwamba ili kuthamini haki za binadamu walau kila chama kitakachoshinda basi kilete mtu mmoja walau mwenye ulemavu wa ngozi. Yupo wapi albino wao hawa? Wabaguzi hawa na inawezekana hata wakati ule wa mauaji wako inawezekana walikuwa wanahusika hawa, yuko wapi? CUF waliwahi kuleta hapa alikuwepo Mheshimiwa Barwany, CCM yule pale wa kwao yupo wapi hawa? (Makofi).
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumze hapa, kwamba usiwaone wanazungumza hivi na nataka nichukue fursa hii kumpongeza sana, nimpongeze sana Mzee Lowassa, Lowassa aligundua hawa wamemchafua sana akaamua kwenda kwao wamsafishe. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mzee Lowasa aligundua walimwita fisadi, walimwita fisadi papa, Edward Lowasa ana akili sana. Mchawi mpe mtoto amlee, akajua nakwenda kwao wanisafishe. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna Mtanzania mwenye akili atakayewasikiliza tena hawa, hivi wewe unakaa na jirani yako mwanaume anakuja anakwambia mke wako malaya, mke wako mhuni unamuacha, asubuhi anamuoa utamwamini tena? Hawa hawaaminiki, hakuna kitu watakachokieleza wakaaminiwa duniani. Kwa sababu wana ndimi mbili kama za nyoka hawa. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanachokisema leo kesho watakibadilisha hawa, ndimi mbili za nyoka…
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana mnawaona leo wanasema hiki, leo wanageuka hivi, nataka nichukue fursa hii kumpongeza Jecha, kwa utaratibu huu wa kila Mzanzibar kuwa Tume ya uchaguzi, Jecha alikuwa sahihi kufuta yale matokeo. (Makofi)
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kila mtu anajifanya Tume, wenyewe unaowaona hapa wameletwa baada ya Tume ya Uchaguzi kuwatangaza ila Mheshimiwa Seif wanamtangaza wao, hawa ni wanafiki wakubwa.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Lusinde, nakushukuru. Muda wako umekwisha.