Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Job Yustino Ndugai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kongwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. JOB Y. NDUGAI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba mwelekeo wa usambazaji umeme Wilayani Kongwa kwa TANESCO na REA kama ifuatavyo:-
(a) Vijiji ambavyo havina umeme kama Pembamoto, Mbagilwa, Bangibanyi, Makole, Nguji, Muungano, Mkoko, Kiteto, Masinyeti nakadhalika.
(b) Vijiji vyote ambavyo bado huduma ya umeme haujafika kwenye sekondari, zahanati, visima vya maji, makanisa, misikiti, vitongoji vilivyoachwa.
(c) Miji midogo inahitaji umeme sana Kibaigwa, Kongwa, Mlali, Mkoka, Sagara, Mbande, Songambele, Pandambili.