Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kuhusu vijiji vya Chipite, Chikindi zahanati, Mbamba, Mbaju, Rahaho, Nanajani pamoja na Mlingura. Vijiji hivi vimepitiwa na waya wa umeme za KVA 33, kuelekea maeneo ya mbele. Nini mpango wa Serikali katika kuhakikisha vijiji hivi vinashushiwa umeme wakati wananchi waliharibu mazao yao mikorosho, miembe na mengineyo?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia katika Kijiji cha Chikindi kuna zahanati pale umeme umepita karibu wanaambiwa walete nguzo kwa shilingi milioni moja. Serikali haioni kama ni muhimu sana kuweka umeme katika maeneo hayo?
Mheshimiwa Naibu Spika, Kijiji cha Nanajani kuna gereza pale, hadi leo wanafuata maji mbali kwa ajili tu ya kukosa umeme. Mitambo ya umeme katika eneo la Masasi ni duni sana. Ningeomba kufahamu mipango ya Serikali katika eneo hilo.