Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nichukuwe nafasi hii kumpongeza kwa dhati Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini Profesa Muhongo kwa weledi wake na uchapa kazi katika Wizara hii ambayo anaimudu sana. Sina shaka na uchapa kazi wa Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninayo machache, naomba uweze kutusaidia sisi Wananchi wa Jimbo la Rufiji wenye wimbi kubwa la umaskini.
Mheshimiwa Naibu Spika, Rufiji ina ardhi yenye rutuba na bonde zuri katika kilimo. Serikali haijawahi kufikiria uwekezaji wa namna yoyote katika bonde hili toka Adam na Hawa mpaka sasa. Hali hii imepelekea uchumi wetu kuwa na hali mbaya. Ukosefu wa maji, hakuna shule za sekondari (Kidato cha Tano) japo kuwa Rufiji ni kubwa kuliko Mkoa mmoja wa Kilimanjaro.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wamepata chuki sana dhidi ya Serikali na hili ni dhahiri na matokeo ya uchaguzi uliopita uliokuwa na ushindani