Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mawaziri, Katibu Mkuu na Wakurugenzi wote wa Wizara hii. Napenda kuchangia yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Buhigwe Makao Makuu tunashukuru umeme umefika na baadhi ya vijiji umeme umefika. Tatizo ni kwamba kati ya vijiji 48 tumefikisha umeme vijiji tisa tu. Tunaomba kipaumbele kwani Mkoa wa Kigoma tumeachwa sana na mikoa na wilaya nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, REA III, tunaomba vijiji vyangu vya Wilaya ya Buhigwe vipate kuwekewa umeme kwani imeanza kuwa kero na siasa kupamba moto kwamba CCM hawawapendi. Kata ambazo hazijapata umeme Buhigwe ni Muhinda, Janda, Munzeze, Mkatanga, Kibwigwa, Kibande, Munyegera, Kilelema, Kajana, Mugera, Bukuba, Kinazi na Rusaba
Mheshimiwa Naibu Spika, jamani tuoneeni huruma.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunawakumbusha kuwa vijiji vyetu ni vikubwa sana na wananchi ni wengi, tunaomba transformer za kutosha kwani vijiji vilivyopata vitongoji, wengine wanalalamika.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaipongeza Wizara kwa uamuzi wa kuzalisha umeme pale Mto Malagarasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, nawatakia ufanisi bora wa kazi zenu.