Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Mbaraka Salim Bawazir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. SALIM M. BAWAZIR: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini kwa kazi nzuri wanazofanya, Makatibu Wakuu na Wakurugenzi wote wa Mashirika yaliyopo Wizara ya Nishati na Madini.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitaelekeza mchango wangu kwa REA. Naomba Serikali iangalie jinsi ya kusambaza umeme katika Vijiji vya Kata zifuatazo – Kata ya Magubike „A‟ na „B,‟ Kidefe, Lumuma, Madoto, Kitete, Lumbiji, Mambaya, Kitonge 1 na 2. Muandi, Chaombele, Ifunde, Mwasa, Kitati, Mzaganza, Mkundi, Dumila Juu, Mkundi Matogolo. Msowero Shule ya Sekondari, Mayambaa Kitongoji cha Mkobwa, Sukutari, Kichangani, Majengo, Mfulu, Madudu, Mbigili, Mabawa, Mateteni, Peapea, Buyuni na Mabatini Unone.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vyote hivyo havijapata umeme wa REA. Naomba Mheshimiwa Waziri utusaidie kupata umeme kwani wananchi wa maeneo hayo wana shida sana. Sambamba na wananchi, umeme pia ni muhimu ufike kwenye shule ya Sekondari ya Msowero. Umeme utasaidia wanafunzi kujisomea nyakati za usiku.
Mheshimiwa Naibu Spika, vinasaba viliwekwa kwa kuwa bei ya mafuta ya taa yalikuwa bei ya chini. Wafanyabiashara wakawa wanachakachua mafuta, lakini sasa bei ya mafuta ya taa iko juu kuliko diesel. Sasa vinasaba vya nini tena? Tunapoteza fedha za Watanzania ambazo zingeweza kutumika kwa kununua madawa na madawati kwa wanafunzi mashuleni.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo lingine ni leseni za mafuta. Upatikanaji wake unasumbua sana wafanyabiashara, masharti ni mengi mno.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.