Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Leonidas Tutubert Gama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. LEONIDAS T. GAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuongelea kuhusu usafirishaji wa makaa ya mawe kutoka machimbo ya Ngaka – Mbinga kupitia Songea Mjini. Makaa ya mawe ni moja ya madini yanayochimbwa katika eneo la Ngaka lililopo Wilayani Mbinga. Uchimbaji wa madini haya ni muhimu sana kwa uchumi na maendeleo ya nchi yetu. Uchimbaji huu unasababisha makaa yasafirishwe kwa njia ya magari makubwa aina ya malori.
Malori haya ni mengi sana na yanasafirisha makaa haya kupitia Mji wa Songea, matokeo ya malori haya kwa Songea Mjini ni:-
(i) Uharibifu wa miundombinu ya barabara ambayo unafanya mazingira kuwa mabovu na mabaya hasa katika maeneo ya Lilambo, Ruhuwiko, Lizaboni, Mjini, Mfaranyaki, Bombambili, Msamala, Mshangano na Shule ya Tanga.
(ii) Magari haya yanapopita huangusha makaa na hata yanapopata ajali. Hali hii inaharibu mazingira ya kiafya ya wananchi wa Songea. Hii ni athari ya kiafya ya wananchi wangu wa Songea Mjini.
(iii) Magari haya yanasababisha msongamano mkubwa wa magari Mjini Songea na makelele kwa mingurumo mikubwa ya malori haya ambayo ni kero kwa wananchi wangu.
(iv) Songea Mjini hakuna eneo maalum la kuegesha magari haya ama yakiwa yamebeba makaa ya mawe au yakiwa yanajiandaa kwenda kubeba makaa ya mawe. Madereva hulazimika kuegesha kwenye maeneo yasiyostahili kama kwenye vituo vya mafuta na kadhalika na hivyo kusababisha kero kwa wananchi wengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na yote haya, je, Manispaa ya Songea ambayo ndiyo inayofanya kazi zote za marekebisho ya matatizo yanayosababishwa na malori haya inanufaika vipi na machimbo haya ya makaa ya mawe?
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niishauri Serikali iamue kujenga njia ya mchepuko ili kuepusha madhara hayo kwa kupita nje ya Mji wa Songea. Zipo barabara za asili zinazotoka eneo la Peramiho na kuunganisha na barabara kuu ya Songea – Dar es Salaam kupitia Njombe ambazo ni barabara ya Peramiho – Shule ya Tanga na barabara ya Peramiho – Madaba. Aidha, ufumbuzi wa kudumu ni mpango wa utengenezaji wa reli ya Mtwara – Mbambabay kupitia Liganga na Mchuchuma.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.