Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuongelea kuhusu umeme katika visiwa vidogo na vikubwa vilivyopo Ukerewe. Pamoja na sera ya Serikali kusambaza umeme vijijini bado kuna tatizo la nishati ya umeme katika visiwa mbalimbali vilivyopo katika Jimbo la Ukerewe. Nashauri Wizara itoe kauli ya matumaini juu ya upatikanaji wa umeme katika visiwa hivi kwa sababu nishati hii ni kichocheo cha maendeleo kwenye visiwa hivi.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ambayo line kubwa za umeme zimepita basi vijiji hivyo vipatiwe nishati mbadala ya kushuhudia tu nyaya zimepita kwenye maeneo yao. Pia pale ambapo tayari kupitia REA umeme umefika kwenye eneo basi wananchi wanaohitaji nishati hii wapewe haraka badala ya kuzungushwa hadi wanakata tamaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Kisiwa cha Ukara umeme wa jua kupitia kampuni binafsi ya JUMEME umewekwa lakini gharama za nishati hii ni kubwa mno kiasi kwamba wananchi wanashindwa kuimiliki. Naomba Wizara iingilie na kuhakikisha kuwa gharama zinakuwa nafuu.