Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Waziri kwa hotuba yake nzuri iliyojaa matumaini ya Watanzania kujitoa kwenye vibatari hadi kuwa na umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo langu la Lushoto tunakushukuru baadhi ya vijiji vimepata umeme. Pia ametuma timu yake imeenda kupima maeneo yote ambayo yamekosa umeme wa REA II na kuwahakikishia wananchi wangu kuwa Jimbo la Lushoto litapata umeme kwa yale maeneo yote yaliyobaki. Mungu ambariki sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimwombe Mheshimiwa Waziri kwa kuwa wananchi wangu wameshakuwa na matumaini makubwa juu ya suala zima la umeme, niendelee kumwombea kwa Mwenyezi Mungu ili aweze kutimiza ahadi yake hiyo ili ifikapo 2020 wananchi wangu waendelee kuamini Serikali yao ya Chama cha Mapinduzi. Pia napenda kuorodhesha maeneo ambayo hayajapata umeme pamoja na kwamba maeneo mengine ya kata na vitongoji yameshapata umeme. Kata ambazo hazina umeme pamoja na vijiji vyake ni kama ifuatavyo:-
(i) Makanya yote;
(ii) Ngwelo baadhi ya vijiji;
(iii) Kilole baadhi ya vijiji;
(iv) Kwekanga baadhi ya vijiji;
(v) Gare baadhi ya vijiji;
(vi) Kwemashai baadhi ya vijiji;
(vii) Ubiri baadhi ya vijiji;
(viii) Magamba baadhi ya vijiji;
(ix) Kwai baadhi ya vijiji;
(x) Mgambo baadhi ya vijiji;
(xi) Mbwei baadhi ya vijiji;
(xii) Malimbwi baadhi ya vijiji;
(xiii) Lushoto baadhi ya vijiji;
(xiv) Mlola baadhi ya vijiji; na
(xv) Ngulwi baadhi ya vijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.