Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nishukuru kwa kunipa nafasi kupitia uchangiaji wa njia ya maandishi ili niweze kuwasilisha mambo machache yanayohusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme hususani katika Jimbo la Iramba Mashariki, Wilaya ya Mkalama na Mkoa wa Singida.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kitabu cha hotuba ya Waziri, ukurasa wa 20 imeelezwa kuwa katika awamu ya III ya REA vijiji vyote ambavyo havikupata umeme vitapatiwa nishati hiyo. Hata hivyo, utekelezaji wa mradi wa REA unaoendelea umeacha maswali mengi kwa Mbunge na wananchi wa Mkalama kwa misingi ifuatayo:-
(i) Vijiji vingi viliachwa yaani havimo katika orodha ya kupata umeme.
(ii) Vijiji vichache vilivyopitiwa na mradi huo nguzo zimepita barabarani na hazijaingia mitaani zilipo huduma za zahanati, shule na huduma zingine za jamii ikiwemo makazi ya wananchi. Mfano ni vijiji vya Kinyangiri, Gumanga, Lambi na Iguguno.
(iii) Vijiji vingi na vikubwa ambavyo baadhi havimo katika mradi huo ni hivi vifuatavyo:-
(a) Kirumi (hospitali na zahanati) Kata ya Matongo;
(b) Mwangeza, Dominiki;
(c) Mwanga, Kidarafa, Kidigida, Msiu;
(d) Kata yote ya Miganga (Miganga, Ipuli)
(e) Mtamba, Kinandili;
(f) Senene, Iguguno Shamba, Mpako;
(g) Yulansoni;
(h) Nyahaa, Mkiwa, Igengu;
(i) Kikhonda, Kinampundu, Mdilika; na
(j) Gumanga kilipo kisima cha maji kilometa 5.
Mheshimiwa Naibu Spika, nina ushauri ufuatao:-
(i) Mradi wa REA upanuliwe ili uweze kufika katika maeneo niliyotaja;
(ii) Nguzo ziongezwe na zifike zilipo huduma muhimu siyo kuishia barabarani;
(iii) Wananchi wanaopitiwa na mradi wa umeme walipwe fidia kwa wakati, mfano wananchi wa Kijiji cha Tamali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.