Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Naibu Spika, sina budi kumpongeza Profesa Sospeter Mwijarubi Muhongo na Naibu wake Waziri Mheshimiwa Dkt. Medard Matogolo Kalemani na Katibu Mkuu wa Wizara Profesa James Pallangyo Justin William Ntalikwa kwa kazi nzuri ya kuhakikisha wanawapatia Watanzania umeme kwa kuzima kibatari majumbani.
Mheshimiwa Naibu Spika, sina budi kushukuru katika Jimbo langu la Kibiti vipo baadhi ya vijiji tumeshapata umeme kwenye phase I ambapo ni 18 kati ya 40. Vijiji hivyo ni Kibiti, Nyamisati, Mchukwi, Mlanzi, Mahenge, Bungu, Songa na vinginevyo lakini umeme wake bado unasumbua wakati wote. Naomba Serikali yangu sikivu ya Chama Tawala kuliangalia suala hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna vijiji ambavyo umeme umefika lakini bado haujawaka. Vijiji hivyo ni Mwangia, Mngaru, Kimbuga, Miwaga, Ngulakula, Uponda Uchembe na Jaribu Mpakani. Vijiji hivi miundombinu ya umeme imekamilika lakini bado kuwashwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna vijiji ambavyo havifanyi vizuri katika suala zima la ukandarasi na miundombinu yake haiendi kwa kasi. Wakandarasi katika maeneo haya kazi zao zimesimama kwa muda mrefu. Naomba wananchi wa Jimbo la Kibiti tuelezwe tatizo ni nini. Vijiji hivyo ni Nyamatanga, Rungungu, Ruaruke Kikale, Mtunda na Muyuyu.
Mheshimiwa Naibu Spika, fidia ya mradi wa umeme wa kilowati 400 toka Somanga - Dar es Salaam – Kinyerezi. Lipo tatizo la fidia katika mradi huu kwani cha ajabu yapo maeneo wameshalipwa lakini katika Jimbo langu la Kibiti bado kabisa. Naomba majibu kutoka kwa Waziri mwenye dhamana fidia hii tutalipwa lini na tutalipwa kwa kiwango kile au tutafanyiwa tena valuation mpya kwani umeshapita muda mrefu. Maeneo ambayo wameshafanyiwa malipo ni Dar es Salaam, Kipunguni Kivule.
Mheshimiwa Naibu Spika, umeme maeneo ya delta. Maeneo haya yote ya delta ambayo yana Kata tano za Salale, Msala, Kiongoroni, Maparoni na Mbuchi. Kata hizi zipo kwenye mazingira magumu pembezoni mwa Bahari ya Hindi ambapo vipo jumla ya vijiji 16 sawa na vitongoji 67.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Kibiti vijiji ambavyo havina umeme vipo 40. Naomba Serikali yangu sikivu ya Chama cha Mapinduzi katika phase III Jimbo langu la Kibiti tupewe umeme. Vijiji hivyo ni Kinyanya, Mkupuka, Nyamwimbe, Bumba Msoro, Pagae, Makima Motomoto, Mjawa, Zumbwini na Tomoni.
Mheshimiwa Naibu Spika, matumizi ya gesi majumbani ni muhimu sana. Kwa hiyo, naiomba Serikali yangu sikivu gesi iondolewe vikwazo kama vipo kwani nishati hii ina mchango mkubwa katika kutunza mazingira kwani itapunguza matumizi ya mkaa, kuni, umeme na mafuta ya taa katika matumizi ya siku majumbani na wananchi wapewe elimu ya kutosha kuhusu matumizi ya gesi na faida zake.
Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika letu la Umeme TANESCO Rufiji lina changamoto kubwa kama ifuatavyo:-
(i) Vifaa vya kisasa vya kufanyia kazi;
(ii) Usafiri;
(iii) Posho za saa za ziada;
(iv) Posho za likizo;
(v) Ukarabati na majengo ya ofisi na nyumba; na
(vi) Kutoa elimu kwa wananchi kuhusu miradi ya REA kwamba haina fidia.